• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YAKABIDHI PIKIPIKI 48 KWA MAAFISA UGANI ARUSHA DC.

Posted on: July 1st, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imetoa pikipiki 48 kwa Maafisa Kilimo, halmashauri ya Arusha, ikiwa ni vitendea kazi kwa Maafisa hao, lengo likiwa ni kuboresha sekta ya Kilimo nchini.

Akizungumza wakati akikabidhi pikipiki hizo, Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango, amewaagiza Maafisa Kilimo kuhakikisha wanatumia pikipiki hizo, kutekeleza majukumu yao kama yalivyo makusudio ya serikali na si vinginevyo.

" Serikali inathamini kazi kubwa mnayoifanya na kuwapa vyombo hivi vya usafiri ili kuwarahisihia utekelazaji wa majukumu yenu kwa wakulima, hatutegemei kuwakuta ofisini, ni jukumu lenu sasa kuwafuata na kuwafikia wakulima kwa haraka na kwa wakati, tunategemea matokeo chanya kwenye sekta ya kilimo katika wailya yetu." Amesisitiza Mhandisi Ruyango.

Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, Mheshimiwa Ojun'gu Salekwa, amekiri kufarijiwa na serikali ya awmu ya sita,  kuwapatia maafisa Kilimo vyombo hivyo vya usafiri, kutokana na mazingira magumu wanayofanyia kazi na kusisitiza kutegemea matokeo chanya kwenye sekta ya kilimo kati halmashauri hiyo.

Hata hivyo mkurugenzi Mtendaji halmasahuri ya Arusha, Seleman Msumi, amewahimiza maafisa hao, kutambua kuwa wamepewa vyombo hivyo vya usafiri kama dhamana, ni muhimu kuvitunza na kuvitumia kwa kazi ya kuwahudumia wakulima katika maeneo yao.

Awali Maafisa ugani hao,  wamemshukuru mheshimiwa rais mama Samia Suluhu na kuipongeza serikali yake ya awamu ya sita kwa kuwapatia pikipiki, ikiwa ni kitendea kazi muhimu kwao, kitakachowarahisishia utekelezaji wa majukumu yao hususani kuwafikia wakulima kwa urahisi zaidi.

Afisa Kilimo kata ya Bwawani, Charles Lyakurwa licha ya kumshukuru mama Samia, amebainisha kuwa pikipiki hiyo ni kitendea kazi muhimu sana kwake, kwa kuzingatia kata yake ya Bwawani ina wakulima wengi wenye mashamba makubwa ambao wanahitaji huduma kutoka kwake kama mtaalamu, bila usafiri wa uhakika ilikiwa ni changamoto kuwafikia kwa wingi wao.

Judith Malya Afisa Kilimo kata ya Ilkiding'a amesema kuwa, awali iliwalazimu kutembea hadi umbali wa Kilomita 20 kuwafuata wakulima, uwepo wa pikipiki utarahisisha na kuwafikia wakulima kwa wakati.

Awali Kiamu Mkuu wa Idara ya Kilimo, halmashauri ya Arusha, Bahati Mtweve, amefafanua kuwa jumla ya pikipiki 48 zimekabidhiwa na serikali kupitia wizara ya Kilimo na kukabidhiwa maafisa Ugani wote 48 kwa majina yao ndani ya halmasahuri, lengo likiwa kuboresha sekta ya kilimo nchini.

KaziInaendelea✍✍
JIANDAE KUHESABIWA

Afisa Kilimo kijiji cha Oloigueruno, Grace Mdaha ( wa kwanza kushoto) akipokea ufunguo wa pikipiki tayari kwa kwenda kuanza kazi,  kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango ( wa kwanza Kulia) , zoezi lililofanyika kwenye ofisi za Makao makuu ya Halmashauri hiyo.









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.