Wananchi wa Kata ya Bwawani wameishukuru Serikali kwa kuwajengea kituo cha Afya kwa gharama ya shilingi milioni 350, fedha kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ambacho kitasaidia kupunguza vifo vya kinamama na watoto kutokana na ukosefu wa kituo cha afya kwenye Kata hiyo.
Wakizungumza wakati ujenzi wa kituo hicho ukiendelea, wananchi hao wamesema kuwa, upatikanaji wa kituo hicho cha afya utaleta manufaa makubwa, kwani hapo awali walikua wanatembea umbali mrefu Kwenda kufuata huduma kwenye kata Jirani ya Nduruma.
“Tulikua tulikuwa na adha kubwa sana ya watu kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 10 Kwenda kufuata huduma za matibabu kwenye kituo cha afya cha Nduruma lakini kwa sasa mradi huu ukikamilika akina mama na watoto watapata huduma hapa”. amesema Patrisia Kaaya, mkazi wa kata ya Bwawani.
Hata hivyo, furaha hio kubwa waliyoipata kutokana na ujenzi wa mradi huo, wananchi hao wamejitokeza kwa wingi kufanya kazi kama sehemu ya nguvu kazi kwenye mradi huo, Huku wakiomba Serikali kuzidi kuongeza miradi mingine ikiwemo ujenzi wa nyumba za walimu pamoja na Nyumba za watumishi wa afya kwenye Kata hiyKwa
Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amesema kuwa mradi huo ukikamilika unatarajiwa kuhudumia Zaidi ya wananchi elfu 18 wa kata hiyo na kata Jirani.“Tutaweza kupunguza vifo vya kina mama na watoto ambao walikuwa wanafuata huduma hizi za kiafya mbali, inapo tokea dharura kwa mgojwa kutembea umbali mrefu inapelekea kuongezeka kwa vifo”. Amesema Mkurugenzi Msumi.
Naye Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Arusha, Grace Makema, amesema kuwa kata ya Bwawani ni moja ya kata ambazo zinapitia changamoto nyingi za huduma za kiafya kutokana na ukosefu wa kituo cha afya hivyo lengo la mradi huo ni kuboresha huduma za kiafya na unatarajiwa kukamilika ndani ya miezAwali
Awali, kata ya Bwawani inazungukwa na Halmashauri za Meru na Simanjiro ambazo wananchi wake wanatarajiwa kupata huduma kwenye kituo hicho cha afya kitakapo kamilika.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.