Serikali kupitia fedha za tozo awamu ya pili, imetoa kiasi cha shilingi milioni 250, kwa ajili ya kuongezea nguvu za ukamilishaji wa upanuzi wa zahanati ya Mwandeti kuwa kito cha Afya, halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru.
Akizungumza na mwandishi wetu, Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amekiri kipokea kiasi hicho cha fedha kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya upanuzi wa zahanati hiyo ya Mwandeti, lengo likiwa ni kuberesha miundombinu ya zahanati hiyo na kuipandisha hadhi kuwa Kituo cha Afya.
Amesema kuwa fedha hizo tayari zimeingizwa kwenye akaunti ya zahanati ya Mwandeti, huku shughuli za utekelezaji wa mradi huo zimeshaanza, lengo likiwa ni uboreshaji wa miundombinu ya vituo vya afya nchini na kuwarahisishia wanachi upatikanaji wa huduma za afya katika maeneo yao.
"Mradi huo unatekelezwa kupitia 'forced akaunt na local fundi', na kiasi hicho cha fedha kitatumika kujenga Jengo la mionzi (X-ray), jengo la kufulia (laundry) na kujenga njia za kutembelea wagonjwa (walk ways), na kiasi cha fedha kitatumika katika ukamilishaji wa jengo la mama na mtoto ( maternity word) na jengo la upasuaji ( theater), majengo ambayo tayari yalishanza kujengwa kwa fedha za awamu ya kwanza". amefafanua mkurugenzi Msumi.
Kaimu Afisa Mipango na Mchumi halmashauri ya Arusha, Alberth Mahoo amefafanua kuwa, kwa mwaka huu wa fedha 2021/2022, serikali ilishatoa fedha kiasi cha shilingi milioni 490 kwa ajili ya upanuzi wa zahanati hiyo ya Mwandeti ili kuwa Kituoa cha Afya, kwa wamu ya kwanza na sasa imetoa kwa awamu ya pili.
Mchumi Mahoo amebainisha mchanganuo wa fedha hizo milioni 490 kwa awamu ya kwanza, kuwa shilingi milioni 150 zilitumika kujenga jengo la mama na mtoto, milioni 250 zilijenga jengo la wagonjwa wa nje na maabara, huku shilingi milioni 90 zikitumika kujenga nyumba ya watumishi ya kuishi familia tatu (3 in 1).
Hata hivyo wananchi wa Mwandeti wameendelea kuishukuru serikali ya awamu ya sita, kwa kuwapa fedha za ujenzi wa kituo cha afya, huduma ambazo hapo awali walitembea umbali mrefu kuzifuata huku wakitumia gharama kubwa za usafiri hasa wakati wa usiku.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.