Na Elinipa Lupembe
Serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na mhe. Rais, Samia Suluhu Hassan, imetoa fedha kiasi cha shilingi milioni 760 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 38 vya madarasa, kwa shule za sekondari halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru.
Kiasi hicho cha fedha kitatumika kujenga vyumba vya madarasa 38 kwa gharama shilingi milioni 20 kwa darasa likiwa na madawati 40 na kufanya jumla ya madawati 1,520 kwa shule 15 za sekondari ikiwa ni maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza ifikapo Januari 2023.
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amethibitisha kupokea kiasi hicho cha fedha, na kuweka wazi kuwa, fedha hizo zimewekwa kwenye akaunti za shule huku ujenzi huo ukiteelekezwa kwa kutumia 'Force Akaunt', sambamba na matumizi ya ramani za madarasa ya 'EP4R'.
Mkurugenzi Msumi amezitaja shule 15 za sekondari ni pamoja na Bangata (1), Einoti (4), Endevesi (1), Kiranyi (2), Likamba (3), Losikito (1), Losinoni (2), Mringa (4), Mukulat (1), Musa (1), Oldadai (11), Olemedeye (1), Oljoro (2), Osiligi (1) na Sambasha (3) na kufanya jumla ya madarasa 38.
Aidha Mkurugenzi Msumi, kwa niaba ya wananchi wa halmasahuri ya Arusha, amemshukuru mheshimiwa Rais kwa kuboresha miundombinu ya shule, ambayo inachochea na kuhamasisha tendo la kujifunza kwa wanafunzi na kufundisha kwa walimu kutokana na mazingira bora ya shule.
"Tunamshukuru sana mama, halmashauri ya Arusha ina wanafunzi 9,711 wanaofanya mtihani wa darasa la saba 2022, tunategemea ufaulu wa asilimia 100, hivyo madarasa hayo, yatasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani ifikapo Januari, 2022". Amefafanua Msumi
Ifahamike kuwa serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 5.3 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 268 kwa shule 88 za sekondari kwa halmashauri 7 za mkoa wa Arusha.
*ARUSHA DC
KaizIendleee
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.