• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA DSW LATOA SAMANI ZA OFISI KWA DAWATI LA JINSIA KITUO CHA POLISI -USA RIVER WILAYANI ARUMERU

Posted on: March 7th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani, shirika lisilo la Kiserikali la DSW limekabidhi samani za ofisi kwa ajili ya ofisi ya Dawati la Jinsia, kwenye kituo cha Polisi cha USA -River wilaya ya Arumeru.

Akizungumza wakati wa kukabidhi samani hizo za ofisi, ikiwemo viti, meza na viti vya wageni, Mkurugenzi wa Shirika la DSW, Peter Owaga, amesema kuwa, shirika limefikia uamuzi huo, mara baada ya kuona juhudi kubwa  na kazi nzuri, zenye matokeo chanya kwa jamii, zinazofanywa na Serikali kupitia Dawati hilo kwa kushughulikia mashauri yanayohusu unyanyasaji wa kijinsia ndani ya wilaya ya Arumeru.

Aidha Owaga amefafanua kuwa, licha ya shirika hilo kutoa elimu na kuhamasisha jamii,  juu ya ukatili wa kijinsia unaofanywa na jamii dhidi ya wanawake na watoto, lakini mafanikio makubwa yametokana na juhudi za Serikali katika kushughulikia kesi na mashauri  ya ukatili wa kijinsia, shughuli zinazofanywa na Dawati la Jinsia kwenye vituo vya polisi nchini.

"DSW imepata matokeo na mafanikio makubwa kwenye miradi inayotekelezwa na shirika ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto, kutokana na juhudi na kazi kubwa inayofanywa na polisi kupitia Dawati  la Kijinsia, matukio ya ukatili yameanza kupungua huku jamii ikanza kuhofia kutokana na sheria kutekelezwa kupitia Dawati la Jinsia" amesisitiza Mkurugenzi Owaga

Naye Msimamizi kituo cha Polisi Usa- River, Afande Juliana Maganga, licha ya kulishukuru shirika la DSW kwa msaada huo, ameweka wazi kuwa kwa sasa Jamii imeanza kutambua umuhimu wa haki za wanawake na watoto kutokana na serikali kuweka Dawati maalum la kushughulikia kesi na mashauri ya ukatili wa kijinsia unaofanyika kwenye jamii.

"Jamii inatambua kazi ya Dawati na tunapokea taarifa za matukio na kuyafanyia kazi kulingana na miongozo, taratibu na sheria, jambo ambalo linasababisha Jamii kuwa makini na kuanza kuogopa kufanya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa kuhofia kuingia kwenye migogoro ya kisheria na Jamhuri" amesisitiza Afande Juliana.

Hata hivyo Afande Juliana amekiri kuwa, kutokana na elimu na juhudi kubwa inayofanya na serikali kwa kushirikiana na Wadau, kwa sasa jamii kuanza kuwa na uwelewa wa pamoja juu ya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, jambo mabalo matukio yameanza kupungua tofauti na hapoa awali, lakini pia jamii inatoa taarifa pindi matukio yanapotokea.

Senorina Frank, Muelimisha Rika na Mwanafunzi wa darasa la VI, shule ya Msingi Olchoruvus kata ya Musa, amesema kuwa kupitia mradi wa Binti na Maendeleo, unaotekelezwa na shirika la DSW katika shule yao, wanafunzi wamepata ufahamu mkubwa juu ya ukatili waliokuwa wakifanyiwa na kutoka na mila na desturi ya jamii yao ya kimaasai, na kuongeza kuwa watoto wameanza kupinga ukatili huo kwa kuelimishana wao kwa wao pamoja na kuwaelemisha wazazi wao kuachana na mila hizo potofu.

"Kupitia Klabu yetu ya Binti na Maendelo shuleni, wanafunzi wengi tumepata ufahamu mkubwa, kwa sasa tunapinga ukatili wa kijinsia, wanafunzi wanajiamini na wanaona umuhimu wa kukataa kukeketwa, kukataa ndoa za utotoni kwa kuwaeleimisha wazazi wao kuachana na mila hizo potofu na wazazi wetu wameanza kuelewa sasa" amesema  Senorina

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani 2022, yenye kauli mbiu ya "Kizazi cha Haki na Usawa kwa Maendeleo Endelevu" - Jitokeze zuhesabiwe, Shirika la DSW limefanya semina na makongamano mbalimbali, yaliyoshirikisha wadau wa maendeleo wakiwemo watoto, wanawake, Jeshi la Polisi, watalamu wa Serikali, waaathirika wa ukatili, waelimisha rika ngazi ya jamii na shule, walimi na wanafunzi, warsha iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa shirika hilo eneo la Tengeru.

ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍












Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.