• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA HACRET LAKABIDHI VIFAA VYA KITAALUMA KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM, SHULE YA MSINGI ILBORU..

Posted on: April 29th, 2023

Na. Elinipa Lupembe

1Shirika lisilo la Kiserikali la HANDICAPPED CHILDREN REHABILITATION TANZANIA (HACRET) linajishughulisha na maendeleo ya watoto wenye mahitaji maalum Mkoani Arusha, limekabidhi vifaa vya kitaaluma kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum, shule ya Msingi Ilboru lengo likiwa ni kuwarahisishia watoto hao tendo la kujifunza na kufundishia.

Mkurugenzi wa Shirika la HACRET, Loy Yamat, wakati akikabidhi vifaa hivyo kwa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, amesema kuwa  lengo la kutoa vifaa hivyo ni kuwapatia wanafunzi wenye mahitaji maalum fursa ya kujifunza kwa uhuru zaidi na kuwasaidia kutimiza ndoto zao za kielimu.

“Tumekabidhi vifaa hivi kuhakikisha watoto wenye mahitaji maalum vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 35 ili kuhakikisha watoto hawa wanakuwa na maaingira ya kujifunzia yakijumuisha na vifaa vya kisasa vya kujifunzia na ufunzaji”. Amesema Mkurugenzi huyo.

Amevitaja vifaa alivyovikabidhiwa ni pamoja na makabati 10, viti na meza, vifaa vya stadi za Maisha na vifaa vya TEHAMA kompyuta mpakato 14,  mashine ya kudurufu 1 na Projecta 1, vifaa ambavyo licha ya kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji katika shule hiyo, vitaongeza chachu ya wanafunzi kujifunza.

Akizungumza baada ya kupokea vifaa hivyo na kuvikabidhi kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Ilboru kitengo maalum, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amelishukiru shirika hilo na kuwataka walimu pamoja na watumishi wote shuleni hapo, kuwasimamia wanafunzi kuvilinda na kuvitunza vifaa hivyo ili viweze kutumika kama vilivyokusudiwa na hatimaye viweze kuwasaidia watoto hao kutimiza ndoto zao.

“Kikubwa ni shukrani sana kwa ndugu zetu wa HACRET, kama tunavyofahamu jamii yetu kwa kiasi kikubwa ilikuwa ikiwaficha watoto wenye mahitaji maalum na ilikuwa inaonekana kama ni mkosi na aibu katika familia, lakini tumshukuru Mungu leo hii Serikali imefanya juhudi na kuhakikisha watoto hawa wanapata haki zao za msingi ikiwemo Elimu”. Amesema Mkurugenzi Msumi.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwl. Philomena Mbilinyi amelishukuru shirika hilo kwa kuwaletea vifaa hivyo, ambavyo vinakwenda kutatua changamoto kubwa iliyokuwepo ya uhaba wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia na kuahidi kuendelea kuvitunza na kuhakikisha vinatumika kwa matumizi fasaha ya kuwaletea wanafunzi hao mandeleo ya kitaaluma.

Hata hivyo wanafunzi hao wamethibitisha changamoto ya waliyokuwa wanakabiliana nayo hapo awali ikiwemo ya kukosa madaftari na kupelekea kuchapwa viboko na walimu ambapo sasa changamoto hiyo imepata mwarobaini.

“Madaftari tutapewa, hapo zamani tulikwa tunasumbuliwa na changamoto tulikuwa tukikosa madaftari na tukienda kuwamba walimu wanasema hawana na madarasani tunatandikwa fimbo, sasaivi tumepata ufadhili tutaendelea na masomo vizuri”. Amesema Mwanafunzi wa shule hiyo mwenye Ulemavu wa Ngozi, Feisal Mohemed.

Awali, hivi karibuni Serikali ilitoa fedha shilingi Milioni 50 kwaajili ya ujenzi wa uzio katika shule hiyo kwaajili ya kuhakikisha usalama wa wanafunzi hao wenye mahitaji maalumu ambapo hadi sasa ujenzi huo umekamilika.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.