• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA KEF LAKABIDHI JENGO LA WATOTO WENYE ULEMAVU SHULE YA MSINGI OLDADAI.

Posted on: July 27th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wadau wa maendeleo sekta ya elimu wa shirika lisilo la kiserikali la Kilimanjaro Education Foundation (KEF) wamejenga darasa maalum kwa wanafunzi wenye ulemavu, kwenye kituo cha Elimu Maalum shule ya msingi Oldadai, halmashauri ya Arusha.

Shirika hilo limefikia uamuzi huo, mara baada ya kujionea, changamoto iliyokiwa inawakabili watoto wenye mahitaji maalum hususani walemavu wa viungo shuleni hapo, kwa kukosekana kwa miundombinu rafiki kwa watoto wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa kukabidhi darasa hilo, Mkurugenzi wa shirika hilo, Bi. Michelle Land, amesema kuwa, baada ya kufadhili mradi wa maji shuleni hapo, waligundua changamoto wanayoipata watoto wenye ulemavu, shuleni hapo na kuamua kujenga jengo maalum lenye miundombinu rafiki, inayojumisha chumba cha darasa, vyoo maalum vya walemavu, mabafu, ofisi ya walimu, samani za ndani pamoja na viti mwendo  mradi ulliogharimu kiasi cha shilingi milioni 48.

Michelle, ameweka wazi kufurahishwa na kitendo cha kukamilika kwa mradi huo, kwa kuwa anaamini malengo ya shirika ya kuwawezesha watoto wenye ulemavu, kusoma kwenye mazingira salama na rafiki yametimia na kuahidi kuendelea kutoa misaada mingine zaidi shuleni hapo.

"Leo nina furaha, kuona darasa hili limekamilika, ninaamini watoto hawa, watafurahia kusoma na kujifunza kwenye mazingira wezeshi kwao, kama wanavyofurahia kwa watoto wengine" Amesisitiza

Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi amelishukuru shirika la KEF, kwa msaada huo wa thamani kwa watoto wenye mahitaji maalum, kwa kuwa utawawezesha watoto hao, kujifunza katika mazingira bora na salama zaidi hasa kwa afya zao.

"Tumepata darasa, kazi imebakia kwa wanafunzi kusoma kwa bidii, na walimu timizeni  jukumu la kuwafundisha watoto hawa wa Mungu, hakikisheni darasa linaendelea kuwa safi kila siku, simamieni watoto kutunza miundombinu hii". Amesisitiza Mkurugenzi Msumi.

Naye Afisa Elimu Msingi, halmashauri ya Arusha, amesisitiza kuwa, uwepo wa mazingira rafiki kwa watoto wenye ulemavu shuleni, kunaongeza ari ya watoto hao kupenda shule pamoja na kujifunza zaidi, na kuwataka walimu kuhakikisha watoto hao, wanafikia ndoto na malengo yao.

Aidha amewataka walimu, pamoja na kutekeleza jukumu lao la kuwafundisha watoto hao, amewataka kuwasimamia wanafunzi kutunza miundombinu hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Mkuu wa shule ya msingi Oldadai, mwalimu David David, licha ya kulishukuru shirika hilo, amesema kuwa hapo awali wanafunzi hao, walikabiliwa na changamoto ya miundombinu ya vyoo na chumba cha darasa, changamoto ambayo kwa sasa imemalizika katika kituo hicho.

Aidha amewata wazazi wenye watoto wenye ulemavu, kuwapeleka watoto hao shule kwa kuwa wanafundishika kama ilivyo watoto wengine na kuwaonya baadhi ya wazazi kuacha kuwaficha watoto hao kwa kuwa serikali imeweka mazingira rafiki ya kujifunzia maalum kwa watoto hao.  

Awali Kitengo cha Elimu Maalum shule ya Msingi Oldadai, kina jumla ya wanafunzi 35 wavulana 19 na wasichana 16 wote wakiwa ni walemavu wa viungo.


SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI

JIANDAE KUHESABIWA✍✍✍


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA MAKABIDHIANO YA MRADI WA JENGO LA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU SHULE YA MSINGI OLDADAI.

Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi na Mkurugenzi wa Shirika la Kilimanjaro Education Foundation, Michelle Land wakikata utepe kama ishara ya kufungua jengo la wanafunzi wenye ulemavu shule ya Msingi Oldadai.


Jengo Maalum la Wanafunzi wenye Ulemavu shule ya Msingi Oldadai, lililojengwa na shirika la Kilimanjaro Education Foundation kwa gharama ya shilingi milioni 48.



Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi akimkabidhi cheti cha shukurani, Mkurugenzi wa Shirika la Kilimanjaro Education Foundation Michelle Land, mara baada ya kukabidhiwa jengo la wanafunzi wenye ulemavu shule ya Msingi Oldadai.



Mkurugenzi wa Shirika la Kilimanjaro Education Foundation, Machelle Land, akihutubia wananchi wa Oldadai wakati wa hafla ya makabidhiano ya  jengo la wanafunzi wenye ulemavu shule ya Msingi Oldadai.








Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA NAFASI ZA UDEREVA TAREHE 28/12/2018 December 19, 2018
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI DUNIANI TAREHE 1-7, AGOSTI 2020. July 31, 2020
  • TANGAZO KWA WANANCHI WOTE MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA PILI 2O20/2021 TAREHE 29.01.2021 January 29, 2021
  • KINGA TIBA YA KICHOCHO NA MINYOO YA TUMBO KWA WATOTO MIAKA 5-14 March 02, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DC ARUMERU AFUNGUA KIKAO CHA BARAZA LA BIASHARA LA WILAYA

    October 19, 2023
  • MBUNGE VITI MAALUM MKOA WA ARUSHA AGAWA MAJIKO YA GESI NA VYERAHANI

    October 17, 2023
  • MAGUNIA 237 YA BANGI YATEKETEZWA ARUMERU

    October 18, 2023
  • SIKU YA MWANAMKE ANAYEISHI KIJIJINI ARUSHA DC

    October 15, 2023
  • Tazama zote

Video

MFUGAJI AKIELEZEA FAIDA ZA UHIMILISHAJI WA NG'OMBE WA MAZIWA - BANDA LA MIFUGO ARUSHA DC
Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.