• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kiwanda cha SUNFLAG Arusha, chatoa msaada, wa vifaa vya kufanyia usafi ARUSHA DC

Posted on: September 9th, 2019

Halmashauri ya Arusha, imepokea msaada wa  vifaa vya kufanyia usafi, vyenye thamani ya shilingi milioni 2, msaada uliotolewa na Kiwanda cha kutengeneza nyuzi na nguo, SUNFLAG  cha Jijini Arusha.

Akizungumza kwa njia ya simu, meneja wa Kiwanda cha Sunflag, Harun Mahundi, amesema kuwa, lengo la kutoa vifaa hivyo, ni kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano, inayosisitiza suala la kufanya usafi wa mazingira, pamoja na kudumisha uhusiano mzuri baina ya kiwanda hicho na halmashauri ya Arusha.

Ameongeza kuwa, ni kawaida ya kiwanda kutumia asilimia kidogo ya faida wanayopata, kurudisha fadhila kwa wateja wake, ambao ndio wananchi, na kuvitaja vifaa hivyo ni pamoja na matoroli, mifagio, mafyekeo, majembe, reki, mikasi, buti, makoti, na vifaa vya kukusanyia taka.

Naye mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera, ameushukuru uongozi wa kiwanda hicho, na kusema kuwa, serikali inathamini michango ya wadau wa maendeleo, ndio sababu imeandaa mazingira mazuri ya uwekezaji kwa faida ya wananchi hasa watanzania wa hali ya chini kiuchumi.

"Nishukuru kiwanda cha Sunflag kwa msaada huu, unaokwenda kusafisha magulio, ambayo kwa kiasi kikubwa yanawahudumia wananchi wetu, wasio na uwezo mkubwa kiuchumi" amesema Dkt. Mahera.

Aidha Afisa Usafishaji na Mazingira, halmashauri ya Arusha, Marlaw Msuya, amesema kuwa, vifaa hivyo vimekuja wakati muafaka, kutokana na changamoto ya uhaba wa vifaa vya kufanyia usafi iliyokuwepo, inayosababishwa na ukubwa maeneo yanayofanyiwa usafi na halmashauri yenyewe kwa sasa.

Nao wafanyakazi wa Idara ya Usafishaji, wamekiri uwepo wa vifaa hivyo utaongeza ufanisi katika kutekeleza majukumu yao ya ukufanya usafi, huku vikiwahakikishia usalama wa afya zao pia.

Abdala Maigisa, amesema kuwa, wanafanya usafi na kukusanya taka kwenye maeneo ya masoko ambapo kuna taka za kila aina, hivyo kutokuwa na vifaa kama glovusi, buti na vizolea taka, mara nyingi huhatarisha usalama wa afya zao na kufanyakazi kwa hofu, lakiji uwepo wa vitendea kazi imara, utaongeza kasi na ari ya kazi.

" Tunasafisha na kukusanya mchanganyiko wa kila aina ya taka, hivyo bila vifaa ni hatari kwa afya zetu, unaweza kuchomwa na taka zenye ncha, unaweza kupata hata maradhi ya kuambukizwa, vifaa hivi vitasaidia kufanyakazi zetu bila hofu" amesema Maigisa.

Halmashauri ya Arusha, kupitia Idara ya Usafishaji na Mazingira, imekuwa mstari wa mbele kutekeleza agizo la makamu wa Rais mama Samia Suluhu la kufanya usafi kila mwisho wa mwezi na kuhakikisha mazingira yote yanakuwa safi kwa afya ya wananchi.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.