• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TAKUKURU ARUMERU YAAZIMIA KUZUIA MIANYA YA UPOTEVU WA MAPATO YA HALMASHAURI.

Posted on: September 30th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Taasisi ya Kuzuia na  Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), wilaya ya Arumeru, imeweka mikakati ya ukusanyaji wa mapato ya halmashauri za wilaya hiyo za Arusha na Meru, lengo likiwa kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya serikali pamoja na kuzuia mianya ya upotevu wa mapato.

Mikakati hiyo imebainishwa na Kamanda Mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Arumeru, Deo Mtui, wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha watalamu, wakusanya mapato na Mawakala wa mapato wa  halmashauri mbili za wilaya hiyo, kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano chuo cha Ualimu Patandi.

Kamanda huyo amesema kuwa TAKUKURU imefuatilia na kuchunguza hali ya ukusanyaji wa mapato na kubaini changamoto za mashine za kielektroniki za kukusanyia mapato 'POS',  ambazo zinaweza kusababisha upotevu wa mapato ikiwemo, wakusanya mapato kutokuweka  fedha benki kwa wakati mara baada ya kukusanya na utaratibu hafifu wa ukusanyaji wa ushuru hasa kwenye minada ya mifugo.

"Tunalazimika kuwa na mkakati wa kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato lakini zaidi kuthibiti upotevu wa mapato hayo, kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za ukusanyaji ikiwemo uwasilishaji wa fedha za Umma kwa wakati, kinyume na hapo ni uvunjifu wa sheria, unaobainisha viashiria vya rushwa"Amefafanu Mtui

Hata hivyo Kamanda huyo wa TAKUKURU amewataka Mawakala wa makusanyo ambao wanadaiwa fedha walizokusanya, kuhakikisha wanaweka fedha hizo kwenye akaunti za halmashauri kabla ya kufikia tarehe 05.10.2022 na kuwaagiza wakurugenzi wa halmashauri hizo kusimamia zoezi hilo ili fedha hizo za serikali ziwe mahali sahihi tayari kwa matumizi ya kuwahudumia wananchi.

Awali wakurugenzi wa halmashauri zote mbili, wameahidi kufanyia kazi maoni na ushauri sambamba na kutekeleza maagizo ya kuimarisha usimamaizi wa ukusanaji mapato huku wakifuatilia wadaiwa sugu ambao hawajaweka fedha hizo kwenye akaunti za halmashauri ifikapo tarehe 05, Oktoba.

Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amebainisha umuhimu wa kikao kazi hicho, kilichozipa fursa halmashauri kujitathmini na kuwa na mikakati thabiti, wakiwa kama Maafisa Masuhuli na wasimamizi wa makusanyo ya mapato ya serikali.

"Tunaishukuru TAKUKURU kwa kikao kazi hiki, kwa kuwa kimetuleta pamoja na kutujengea uelewa wa pamoja wa namna bora ya kuzuia mianya ya rushwa katika ukusanyaji wa mapato ya halmashauri zetu, niahidi kufanyia kazi maelekezo tuliyopewa, yakiwa na lengo la kuimarisha ukusanyaji wa mapato pamoja na matumizi sahihi ya mapato hayo kwa maendeleo ya wananchi wetu" Amefafanua Mkurugenzi Msumi

Kikao kazi hicho cha siku moja, kimewakutanisha wataalamu wa halmashauri, wakiwemo, Maafisa Mapato, Maafisa Biashara, Maafisa TEHAMA, Wakaguzi wa Ndani, Weka Hazina na Mawakala wa kukusanya mapato wakiongozwa na wakurugenzi wa halmashauri hizo hizo mbili.


ARUMERU

TUPO KAZINI✍✍✍


PICHA ZA MATUKIO YA KIKAO KAZI


Mkuu wa TAKUKURU  wilaya ya Arumeru, Deo Mtui akizungumza wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha watalamu, wakusanya mapato na Mawakala wa mapato wa  halmashauri zaArusha na Meru, kwenye ukumbi wa mikutano Chuo cha Ualimu Patandi.



Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi ( aliyesimama) akizungumza wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha watalamu, wakusanya mapato na Mawakala wa mapato wa  halmashauri zaArusha na Meru, kwenye ukumbi wa mikutano Chuo cha Ualimu Patandi.


Afisa Mapato halmashauri ya Arusha, Ephata Swai, akizungumza wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha watalamu, wakusanya mapato na Mawakala wa mapato wa  halmashauri zaArusha na Meru, kwenye ukumbi wa mikutano Chuo cha Ualimu Patandi.



Watalamu wa halmashauri za Arusha na Meru wakiwa kwenye kikao kazi na watalamu wa TAKUKURU, kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha Ualimu Patandi.














Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.