• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA ARUSHA

Posted on: May 29th, 2020

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, anapenda kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa zinazohitajika na wenye nia ya kufanya kazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha kuomba kujaza nafasi wazi za kazi kupitia kibali Kumb.Na. FA.170/371/01/104   cha tarehe 30 April ,2020 kilichoidhinisha nafasi mbalimbali za kazi kama ifuatavyo:

KATIBU MAHSUSI  DARAJA  III ( NAFASI 2)

SIFA ZA MWOMBAJI

Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV waliohudhuria mafunzo ya Uhazili na kufaulu mtihani wa hatua ya tatu.

Awe amefaulu somo la hati mkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja.

Awe amepata mafunzo ya kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali na kupata cheti katika progam za Windows, Microsoft Office, Excel, Internet, Email na Publisher.

  1.2 NGAZI YA MSHAHARA

 Cheo cha Katibu Mahsusi Daraja III kina ngazi ya mshahara wa TGS B1.

.1Kazi  na majukumu ya Katibu Mahsusi Daraja III

Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida.

Kusaidia kupokea wageni na kuwasiili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa.

 Kusaidia kutunza taarifa/ kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika ofisi anamofanyia kazi, na kumuarifu  mkuu wake kwa wakati unaohitajika.

Kusaidia kutafuta na  kumpatia mkuu wake majalada, nyaraka, au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini.

Kusaidia kufikisha maelekezo ya mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao.

Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa maofisa walio katika sehemu alipo, kukusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika.

Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na msimamizi wake wa kazi.


MSAIDIZI  WA KUMBUKUMU DARAJA II ( NAFASI 2)

SIFA ZA MWOMBAJI

Mwombaji awe amehitimu kidato cha  IV au VI  

Awe ametunukiwa cheti (NTA Level 5) cha utunzaji kumbukumbu katika moja ya fani za Afya, Masijala, Mahakama na Ardhi.

NGAZI YA MSHAHARA

Cheo cha Katibu Mahsusi Daraja III kina ngazi ya mshahara wa TGS B1.

2.3 KAZI NA MAJUKUMU YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMU DARAJA III

Kutafuta kumbukumbu/ nyaraka / mafaili yanayohitajika na wasomaji.

Kudhibiti upokeaji , uandikishaji wa kumbukumbu / nyaraka.

Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu,nyaraka katika makundi kulingana na somo husika ( classification and boxing)  kwa ajili ya matumizi ya ofisi.

Kuweka/ kupanga kumbukumbu/ nyaraka katika reki (file racks / cabinets) katika masijala/ vyumba vya kuhifadhia kumbukumbu.

 Kuweka kumbukumbu (barua / nyaraka n.k) katika mafaili.

Kushughulikia maombi ya kumbukumbu / nyaraka kutoka Taasisi za Serikali.

3. MASHARTI YA JUMLA KWA NAFASI ZOTE

Waombaji wote  wawe ni  Raia wa Tanzania na mwenye umri usiozidi miaka 45.

Waombaji  waambatanishe  wasifu (C.V) wenye anuani sahihi, namba za simu sahihi, pamoja na majina matatu ya wadhamini na namba za simu zinazopatikana.

Testimonial “provisional Result” Statement of Result, hati ya matokeo ya kidato cha nne/Sita HAVIKUBALIKI.

Waombaji waliosoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na TCU au NECTA.

Watumishi waliostaafishwa kazi Serikalini  kwa namna moja au nyingine hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali cha mamlaka stahiki.

Waombaji waambatanishe nakala za vyeti vifuatavyo:

Cheti cha kuzaliwa

Cheti cha kuhitimu elimu ya Kidato cha nne (IV) na Sita (VI) kwa wale waliofika kiwango hicho.

Cheti cha taaluma na mafunzo mbalimbali.

Passport size 1

Mwisho wa kutuma maombi  ni tarehe 10/06/2020                                                                                                                                                                                                              

Maombi yatakayowasilishwa  nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili “HAYATAFIKIRIWA”.


MAOMBI YOTE YATUMWE KWA NJIA YA POSTA  KATIKA ANUANI IFUATAYO:

MKURUGENZI MTENDAJI,

HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA,

S.L.P 2330,

ARUSHA.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.