• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TASAF YABADILI MAISHA YA KAYA MASIKINI ARUSHA DC

Posted on: September 25th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

   Wanufaika wa mpango wa kunusuru Kaya Masikini, mradi unaotekelezwa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF, halmashauri ya Arusha wameendelea kuishukuru serikali kupitia mradi huo, wa kuwapatia ruzuku ya fedha kwa ajili ya kujikimu kimaisha.

     Wakizungumza na mwandishi wetu, wakati wa zoezi la kupokea pesa, lililofanyika kwenye vijiji 45 vilivyo kwenye mpango halmashauri ya Arusha, wanufaika hao wamekiri licha ya kuwa fedha hizo ni kidogo lakini, zinawasaidia kupunguza makali ya maisha.

Suzana Mollel mkazi wa Sekei, amesema kuwa fedha hizo zimemuwezesha kujikwamua kimaisha ikiwemo, kutunza familia yake kwa kuwapatia mahitaji ya muhimu ikiwemo chakula na mavazi, sambamba na kununua mahitaji ya shule kwa watoto, jambo ambalo hapo awali lilikuwa ni kikwazo kutokana na uwezo duni aliokuwa nao.

"Ninafamilia ya watoto wanne wanaonitegemea, mume alinitelekeza muda mrefu, maisha yalikuwa magumu sana, zilipokuja hela za TASAF, zimenisaidika kupunguza makali ya maisha, nimeweza kufuga kuku na mbuzi, hali ya uchumi na maisha ya familia vimebadilika, ninaweza kujikimu, tofauti na hapo awali" amesema Suzana.

    Naye Mwenyejiti wa kijiji cha Sekei,  Miriam Lomayani, ameweka wazi kuwa, mradi huo wa TASAF wa kusaidia kaya masikini, umeziwezesha kaya nyingi kujikwamua kimaisha, kutokana na ukweli kwamba kabla ya mpango huo wa TASAF, kuna baadhi ya kaya zilikuwa na hali mbaya kiuchumi.

    "Kwenye kijiji changu zipo kaya zimefanya mabadiliko kupitia pesa hizo, licha ya kwamba ni kidogo, wapo wanakaya waliotumia fedha hizo, kuwekeza kwenye miradi ya ufugaji kuku na mbuzi kilimo cha mbogamboga na biashara ndogondogo, jambo lililobadilisha hali zao za kimaisha za kaya hizo" amethibitisha Mwenyekiti huyo

     Awali jumla ya shilingi milioni 239.3, zimetolewa ikiwa ni ruzuku ya miezi minne, baada ya kukamilika zoezi la uhakiki wa kaya zilizo kwenye mpango, na jumla ya kaya 6,811 zimepokea ruzuku hiyo.






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.