Mheshimiwa Elias Olenaigisa Mollel wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA amechaguliwa tena kuwa Makamu Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Ngaramtoni baada ya kushika nafasi hiyo kwa miaka mitatu tangu kuanza kwa mamlaka hiyo mwaka 2014.
Mh. Elias Mollel ametetea kiti chake baada ya kupata kura 15 kati ya kuta 25 zilizopigwa na kumshinda mpinzani wake Mhe. Rose Enock mwenyekiti viti maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyepata kura 10.
Mtendaji Mkuu Mamlaka ya Mji Mdogo Ngaramtoni ndugu Sophia Shoko amemtangaza Mh. Elias Olenaigisa Mollel ambaye ni Mwenyekiti wa kitongoji cha Namayani kata ya Kiranyi kuwa Makamu Mwenyekiti kwa kipindi cha mwaka mmoja baada ya kupata kura 15 na kumshinda Mhe. Rose Enock aliyepea kura 10 kati ya kura 25 zilizopigwa.
Uchaguzi huo umefanyika wakati wa Mkutano Maalumu wa mwaka wa Baraza la Mamlaka hiyo na kufanya uchaguzi wa Makamu Mwenyiki wa baraza hilo ambapo kisheria huchaguliwa kila baada ya mwaka mmoja.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.