• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

UELEWA MDOGO WA WAZAZI CHANZO CHA NDOA NA MIMBA ZA UTOTONI

Posted on: October 4th, 2019

Vijana wa shule ya sekondari Musa, halmashauri ya Arusha, wameweka wazi kuwa, uelewa mdogo wa jamii hasa wazazi, juu ya afya ya uzazi, imekuwa ni chanzo cha ndoa na mimba nyingi za utotoni.

Wakizungumza wakati wa mdahalo wa Afya ya uzazi kwa vijana, uliofanyika shule ya sekondari Musa, mdahalo uliohusisha wanafunzi wote wa shule hiyo, wamesema kuwa, licha ya changamoto nyingi zinazowakabili vijana,  bado uelewa mdogo wa vijana juu ya afya ya uzazi, umesababisha ndoa za utotoni na vijana kujikuta kwenye changamoto nyingi za kimaisha.

Wamefafanua kuwa, mara nyingi vijana hushauriana wao kwa wao, juu ya mabadiliko yao ya kimwili yanayoambatana na kuanza mahusiano ya kimapenzi,  kwa kupeana taarifa zisizo sahihi, jambo ambalo husababisha mimba zisizotarajiwa pamoja na ndoa za utotoni.

Wameongeza kuwa, kutokana na mila na desturi za jamii zao, inaonesha wazi kuwa, hata wazazi hawana uelewa wa kutosha juu ya afya ya uzazi kwa vijana pamoja na mabadiliko ya kimwili kwa vijana jambo ambalo linasababisha vijana kubaki njia panda na pengine kushindwa kufikia malengo yao kwa kukatiza ndoto zao.

Wanafunzi hao wakwenda mbali zaidi na kusema kuwa, endapo wazazi wangekuwa na uelewa sahihi, juu ya afya ya uzazi kwa vijana, wasingewalazimisha  wasicha kuolewa wakiwa na umri mdogo kwa kuhofia wasichana hao kupata mimba kabla ya ndoa.

Kadhalika katika mdahalo huo, vijana walipata fursa ya kujadili kwa kina juu ya afya ya uzazi na changamoto za mabadiliko ya kimwili zinazosababisha mihemko na namna ta kukabiliana na hisia.

Hata hivyo, halmashauri ya Arusha kupitia mradi wa TCI - TUPANGE PAMOJA , unaotekelezwa na shirika la JHPIEGO -  Tanzania, wameanzisha huduma Rafiki kwa Vijana, huduma zinazotolewa bure kwenye zahanati na vituo vya afya na kuwataka vijana kwenda kwenye zahanati kupata elimu zaidi juu ya afya ya uzazi kwa vijana.

Afisa Afya Shuleni, halmashauri ya Arusha, Niya Mtaki akiongoza mdahalo juu ya afya ya uzazi kwa vijana kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Musa 

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Musa wakifuatilia mijadala kwenye mdahalo wa afya ya uzazi kwa vijana uliofanyika shuleni hapo.

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Musa wakijifunza kwa picha namna ndoto zao zinavyokatizwa wakati wa mdahalo wa afya ya uzazi kwa vijana uliofanyika shuleni hapo.

Mratibu mradi wa afya ya uzazi na Uzazi wa Mpango shirika la JHPIEGO, Waziri Njau, akitoa mada juu ya Uzazi wa Mpango na dini za kikristo na kiislam, wakati wa mdahalo wa afya ya uzazi kwa vijana, shule ya sekondari Musa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.