• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Ujenzi wa miundombinu ya mradi wa maji wa vijiji vitano wafikia asilimia 35%

Posted on: April 4th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Timu ya watalamu wasimamizi wa mradi wa maji wa vijiji vitano, maarufu kama mradi wa maji wa WaterAid, imetembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya mradi huo ulioanza kutekelezwa mapema mwezi Januari, 2019.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi, wakati wakati wa ziara hiyo, Mhandisi Mkazi wa shirika la WaterAid Tanzania, Mhandisi Jailos Chilewa amesema kuwa mpaka sasa ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 35, ikijumuisha ujenzi wa matanki ya kuhifadhia maji, nyumba za kusimikia mitambo ya kutibu maji, nyumba za kuhifadhia pumpu, usambazaji wa mabomba, ujenzi wa vituo vya kuchotea maji (DPs) pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji Emurtoto. 

Mhandishi Chilewa amefafanua kuwa, mradi huo umegawanywa kwenye kandarasi nne,  kutokana na ukubwa wa mradi na kuainisha kuwa,  Lot I ya mradi inatekelezwa na kampuni ya STC Construction Company Ltd, ambao wamefikia asilimia 20%, Lot II unajengwa na  kampuni za Advance Company Ltd & Meero Contractors Ltd na umefikia asilimia 59%,  Lot III unatekelezwa na Kampuni ya ASSES Ltd ambao wamefikia asilimia 78%, huku Lot IV ukitekelezwa na Kampuni ya Daviss and Shirtliff waliofikia asilimia 21%

Ameongeza kuwa licha ya utekelezaji wa ujenzi kuendelea vizuri na kufikia asilimia hizo, bado wakandarasi hao wako nyuma ya muda, kulingana na muda wa kwenye mikataba yao, hali iliyosababishwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya kimazingira kwa baadhi ya maeneo.

Hata hivyo timu hiyo imewaagiza timu ya watalamu wasimamizi wa ujenzi, kuongezeka kwa kasi ya usimamizi na kuhakikisha wakandarasi hao, wanafanya kazi usiku na mchana pamoja na kuwawezesha kukabiliana na aina yoyote ya changamoto zinazojitokeza wakati wa ujenzi wa mradi huo.

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arudha Dkt. Wilson Mahera amesema kuwa, wameweka mkakati wa kuhakikisha watalamu hao, wanawasimamia kwa karibu wakandarasi hao na kushirikiana nao kama timu ili kutatua changamoto zitakazojitokeza wakati wa ujenzi kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata maji kama Serikali ilivyokusudia.

Naye mkurugenzi wa shirika la WaterAid Tanzania, Dkt. Ibrahim Kabole amewasisitiza wakandarasi wanaojenga mradi huo kuwa, licha ya changamoto zote zinazojitokeza wakati wa ujenzi wa mradi huo, lengo kubwa la shirika hilo na wafadhili wa mradi huo, ni wananchi wa vijiji lengwa, kupata maji safi na salama kabla ya mwaka huu wa fedha kukamilika.

" Pambaneni na changamoto zote ' but at the end of the day wananchi wanatakiwa kupata maji safi na salama, hilo ndio lengo la wafadhili DFID na lengo letu kama wasimamizi wa mradi" amesisitiza Dkt. Kabole.

Mradi wa maji wa vijiji vitano, unaotekelezwa na shirika la WaterAid Tanzania, kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya nchini Uingereza 'DFID' kwa gharama ya shilingi bilioni 8.4, umelenga kuhudumia  takribani watu 50,000 wa vijiji vya Lengijave, Olkokola na vitongoji vya Seuri, Ekenywa na Ngaramtoni, na unategemea kukamilka mwishoni mwa mwaka huu wa fedha, ifikapo mwezi Juni 2019.







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.