• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIJANA WAKIRI WAZAZI KUWA WAKALI WANAPOULIZWA JUU YA MABADILIKO YA MAKUZI NA UZAZI KWA VIJANA

Posted on: September 20th, 2020

Na. Elinipa Lupembe

    Vijana wamekiri kutokuwa na taarifa sahihi juu ya masuala ya afya ya uzazi kwa vijana, kutokana na mila na desturi za jamii zao, zinazolazimisha wazazi kuficha taarifa za uzazi, wakiamini kuwaweka vijana wazi ni kuwaruhusu kujiingiza kwenye vitendo vya ngono.

    Vijana hao wameweka wazi mtazamo huo, wakati wa mdahalo uliowahusisha wanafunzi wa shule ya sekondari Kiranyi, halmashauri ya Arusha, mdahalo ulioendeshwa na timu ya watalamu wa TCI - Tupange Pamoja, halmashauri ya Arusha.

     Wanafunzi hao wamesema kuwa, wazazi wamekuwa wakali kwa vijana huku wakishindwa kiwapa watoto wao  taarifa sahihi za masuala ya uzazi na mabadiliko ya makuzi yanayowakabili, na kubaki wakiwakaripia pale wanapouliza matokeo ya mabadiliko hayo, jambo ambalo linasababisha vijana wengi kupata taarifa za uzazi kwa marafiki na kujikuta wakijiingiza kwenye vitendo vya ngono na kuzimisha ndoto zao.

    "Unakuta kijana unamuuliza mzazi, mimi nnatatizo flani yanayotokana na mabadiliko ya makuzi, mzazi anaanza kukugombeza umeanza umalaya, hiyo ni tabia mbaya, unaniabisha, kwenye ukoo wetu hakuna mtoto amewahi kusema hivyo, mzazi hakwambii ukweli, jambo linalotufanya tukaulize kwa marafiki ambao nao hawajui vizuri na kujikuta vijana wengi wanajiingiza kwenye ,asuala ya ngono, ulevi na uvutaji bangi, jambo ambalo mzazi angekwambia ukweli kama ninyi mnavyotwambia, matatizo mengi yasingetokea",Wamesema Vijana hao.  

      Aidha vijana hao wameitaka jamii na wazazi, kutoa elimu kwa vijana juu ya mambadiliko ya makuzi na uzazi ili waweze kutambua mabadiliko hayo vizuri na namna ya kukabiliana na mihemko inayoyokana na mabadiliko hayo.

      Hata hivyo, katika mdahalo huo, watalamu waongoza mjadala, walipata wasaa wa kuwapa elimu ya makuzi na mabadiliko ya via vya uzazi kwa vijana, afya ya uzazi na uzazi wa mpango, na jinsi ya kukabiliana na mihemko ya ujana inayotokana na mabadiliko ya makuzi,  jambo ambalo limewafanya vijana hao, kuona umuhimu wa wazazi na jamii kuwafundisha kwa uwazi, ili waweze kukabiliana na mihemko ya ujana.

    Watalamu hao wamewataka vijana hao, kufika kwenye vituo vya kutoplea huduma za afya, kupata ushauri juu wa Afya ya Uzazi kupitia HUDUMA RAFIKI KWA VIJANA, huduma zinazotolewa bure kwa na kwa siri kwa vijana, huduma ambazo zitawapa uelewa mpana juu ya afya ya uzazi na namna ya kukabiliana na mihemko na vishawishi katika kipindi chote cha ujana.

      Mradi wa TCI-Tupange pamoja unatekelezwa kwa ushirikiano wa halmashauri ya Arusha na shirika la JHPIEGO kwa ufadhili wa mfuko wa  Bill&Melinda Gate wa nchini Marekani.


 PICHA ZA MATUKIO YA MDAHALO WANAFUNZI SEKONDARI KIRANYI.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.