Na Elinipa Lupembe
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023, Ndugu Abdallah Shaib Kaim amewataka vijana nchini kutumia fursa ya mikopo isiyokuwa na riba inayotolewa na serikali kuwekeza katika miradi ili kujikwamua kiuchumi na kukabiliana na changamoto ya ajira nchini.
Akikagua mradi wa Vijana wa Kidali Youth Group kata ya Mwandet, wanaojishughulisha na biashara ya ufugaji wa kununua na kuuza mifugo, waliopewa mkopo wa shilingi milioni 10 kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri amesema kuwa, serikali inayodhamira njema kwa vijana wakitanzania hivyo kutumi fursa hiyo adhimu ambayo itawakwamua kiuchumi na kijamii pia.
Amesema kuwa serikali yao ya awamu ya sita inawajali vijana,, ni vema vijana kutumia fursa hiyo kupambana na hali duni ya maisha huku wakitambua kuwa Jemadari Dkt Samia Suluhu Hassan kama mama yao anatamani mapinduzi ya kifkra, kijamii na kiuchumi kutoka kwa vijana ambao ndio nguzo ya Taifa la Tanzania.
"Nikiwa kama kijana ninafurahia na ninafarijika sana, Mheshimiwa Rais licha ya kutumia fedha nyingi kutekeleza miradi mikubwa na ya kimkakati ya maendeleo nchini, hakuwaacha nyuma vijana, basi na sisi kama vijana tujivunie fursa hiyo na tusimuangushe mhesimiwa Rais , tufanye kazi bila kuchoka ili kulijenga Taifa letu la Tanzania" Ameweka wazi kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa.
Aidha amezitaka halmashauri kupitia watalamu wake, kuendelea kuwasimamia vijana hao kuendesha miradi yao ili kuwa na nidhamu katika katika matumizi ya fedha ili mraci hiyo iweze kukua, na kuongeza kuwa halmashauri ziangalie namna ya kuwaongezea fedha vijana wenye uthubutu ili kukuza mitaji yao.
Hata hivyo amewapongeza vijana wa kikundi cha Kidali Youth kwa uthubutu na ubunifu wa biashara hiyo na kuwataka kusimamia vema kazi yao kwa kuwa itaongeza pato la mtu mmoja mmoja, familia na hatimaye Taifa.
KAULI MBIU: " TUNZA MAZINGIRA, OKOA VYANZO VYA MAJI KWA USTAWI WA VIUMBE HAI KWA UCHUMI WA TAIFA"
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.