• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIKUNDI VYA WALENGWA WA TASAF VYAINUA UCHUMI WA KAYA

Posted on: June 27th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Wanufaika wa mpango wa Kunusuru Kaya Masikini, mradi unaotekelezwa Serikali kupitia Mfuko wa Maendelo ya Jamii -  TASAF III awamu ya pili, wameanza kunufaika kiuchumi kupitia vikundi vya kuweka na kuwekeza, vikundi vilivyoviunda na walengwa hao, halmashauri ya Arusha.

Walengwa hao wa kijiji cha Oltulelei kata ya Ilboru, wameweza kuinua vipato vya familia zao kwa kujipatia mitaji ya kuanzisha miradi midogo midogo, kupitia programu ya vikundi vya TASAF vya kuweka, kuwekeza na kukopa.Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye maeneo ya biashara zao, wana kaya hao wamethibitisha kuwa, licha ya kupokea fedha za ruzuku ya mwezi, lakini pia walijengewa uwezo wa kuanzisha vikundi vya kuweka na kukopa kupitia fedha za ruzuku wanazopokea.

Janeth John  mlengwa na mwenyekiti wa kikundi cha UPENDO -TASAF anayemiliki genge la kuuza mbogamboaga  kwa sasa, amesema kuwa watalamu waliwajengea uwezo wa kuanzisha vikundi vya kuwekeza pesa kutokana na ruzuku wanayoipa kutoka TASAF,na bada ya kuanzisha kikundi kimewawezesha kupata mitaji na kuongeza kuwa kila mwanakukundi ameshaanzisha biashara yake sasa Kikundi chetu kina wana wanachama 10, tulianza tukiwa na hofu sana, lakini kikundi kimetuwezesha kupata mitaji ya kuanzisha biashara, biashara ambazo zimepunguza ugumu wa maisha, biashara zimewawezesha wanakikundi hao kuwekeza, kukopa na kurejesha kwa wakati, na kuongeza kuwa, walipoanza kikundi wengi wao hawakuwa na biashara, na kwa sasa wanachama wote wana biashara, biashara ambazo zimewawezesha kujimudu kimaisha kwa kila mmoja mwanakikundi.

"Hapo mwanzo hatukuamini kama jambo hili kama litawezekana, kutoka na kiasi cha oesa tunachopokea, lakini tumeweza kugonga hisa kila wiki, tuna mfuko wa jamii ambao tunasaidiana kutatua changamoto za kijamii kama msiba na ugonjwa, lakini zaidi tumeweza kukopeshana na kupata mitaji, inayotuwezehsa kuendelea kuweka akiba, kukopa na kupata marejesho, huku faida ya biashara ikituwezesha kuhudumia famialia zetu " amesisitiza Janeth.

Rabisante Mwanga, mwanakikundi cha UPENDO  na mama wa watoto watatu, amebainisha kuwa, kupitia kikundi chao cha UPENDO TASAF, ameweza kupata mtaji wa shilingi 150,000 wa kuuza mitumba, mradi ambao unampatia kipato cha kumudu maisha yake na familia yake huku akiwa na matarajio ya kukuza mtaji na kuanza kununua mitumba kwa jumla maarufu kama 'belo'.

Dina Yoram, mlengwa anayemiliki  genge na sehemu ya kuchoma samaki na mihogo, amefafanua kuwa, Kikundi chao kimewawezesha kuongeza kipato cha familia yake, na kumfanya kumudu mahitaji ya muhimu kwa familia yake na kuwataka wanawake waaibweteke badala yake kutumia futsa hizo za vikundi kuanzisha biashara ili kupambana na hali ya umaaikini.

Hata hivyo Dina Emson, amewaka wazi kuwa kabla ya kuanza kupokea pesa za TASAF alikuwa na ujuzi wa kusuka, akisuka wateja wake eneo lisilo rasmi, baada ya kujiunga na kikundi cha TASAF amefanikiwa kufungua saloon, eneo ambalo limemuwezesha kupata wateja zaidi, mtaji ambao unamudu kulipa kodi ya pango pamoja na kuhudumia familia yake.

"Nilikuwa na ujuzi wa kusuka nawafuata wateja nyumbani, jambo ambalo lilinigharimu nauli ya kwenda na kurudi, kwa sasa wateja wangu wananifuata hapa hapa saloon kwangu, kadri siku zinavyokwenda natarajia kuweka vifaa vyote vya saloon na saloon yangu iwe kubwa zaidi"amesistiza Upendo.

Mpango wa Kunusuru kaya masikini, wenye lengo la kukuza pato la familia, umekuwa na programu ya vikundi vya kuweka na kuwekeza kwa walengwa walio kwenye mpango ili kukuza uchumi wa kaya
program ambayo imeanza kuzaa matunda kwa baadhi ya Kaya hizo.

SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI

JIANDAE KUHESABIWA 23. 8.2022

Janeth John, mlengwa na mwenyekiti wa kikundi cha UPENDO - TASAF akiwa kwenye genge lake la mbogamboga, biahsara ambayo mtaji wake  ameupata kutokana na kikundi cha kuweka na kuwekeza.


Rabisante Mwanga, mlengwa na mwanakikundi cha UPENDO - TASAF akitembeza biasha yake ya kuuza nguo za mitumba, mtaji ambao ameupata kutokana na kikundi cha kuweka na kuwekeza.



Genge la Dina Emson, mlengwa na mwanakikundi cha UPENDO - TASAF, genge ambalo  mtaji wake ameupata kutokana na kikundi cha kuweka na kuwekeza.


Dina Emson, mlengwa na mwanakikundi cha UPENDO - TASAF akimsuka mteja ndani ya saloon yake, biashara ambayo mtaji wake ameupata kutokana na kikundi cha kuweka na kuwekeza







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.