• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Viongozi watakiwa kuhamasisha wananchi kuthamini miradi ya maendeleo katika maeneo yao

Posted on: April 13th, 2018

Viongozi wa ngazi za vijiji,vitongoji na kata, halmashauri ya Arusha wametakiwa kutoa elimu kwa wananchi wanaowaongoza ili waweze kuithamini miradi ya maendeleo, inayotekelezwa katika maeneo yao.     

Rai hiyo imetolewa na Mhandisi wa Maji mkoa wa Arusha, Mhandisi Joseph Makaidi, wakati akiwasilisha mrejesho wa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa maji wa vijiji vitano, unaofadhiliwa na Idara ya Maendeleo ya nchini Uingereza 'DFID' kwa gharama ya shilingi bilioni 4.5.     

Mhandisi Makaidi amesema kuwa, viongozi wa jamii wanao wajibu wa kuwaelimisha wananchi wao, kutambua miradi hiyo kuwa ni mali yao pamoja na kuwashirikisha katika hatua mbalimbali za maamuzi kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo, inayotekelezwa kwenye maeneo yao.  

 " Kama wananchu hawashirikishwi kikamilifu kuanzia mradibunaanza na hatua mbalimbali za mradi husababisha wananchi kuihujumu miradi wakati wa utekelezaji na pia katika uendeshaji wa miradi, miradi mingi imekwama kutokana na wananchi kutokuwa na taarifa sahihi za miradi hiyo" amesema Mhandisi huyo.         Ameongeza kuwa, miradi mingi itakuwa endelevu, endapo wananchi wataifahamu kuanzia mwanzo, hatua zote za utekelezaji mpaka kukamilika kwake.        Hali hii itawapa nafasi wananchi kuisimamia miradi hiyo kwa dhati, huku wakifahamu na kutambua kuwa miradi hiyo ni mali yao.    

Naye diwani wa kata ya Olkokola,na aliyekuwa mwenyekiti wa kikao kazi hicho, mheshimiwa Kalanga Laizer amesema kwamba,kutokana na ushirikishwaji wa wananchi katika hatua zote za mradi wa maji wa vijiji vitano, jamii imeridhika hasa katika ushirikishwaji ulivyoanza na vikao vya wananchi kujengewa uwezo na kuwa na uelewa wa pamoja juu ya mradi huo.          

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera, ameikumbusha jamii kutambua umuhimu wa utunzaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, sambamba na kukubali kukabiliana na changamoto zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi na wakati wa uendeshaji wa mradi pia.      

Hata hivyo Mkurugenzi Mahera, amewahakikishia viongozi na wananchi wa halmashauri ya Arusha usimamizi thabiti wa utekelezaji wa miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya halmashauri licha ya kuwepo changamoto nyingi wakati wa utekelezaji wa miradi.     

Aidha Dkt. Mahera ameupa kipaumbele mradi huu mpya wa maji wa vijiji vitano, ambao kimsingi utasaidia kupunguza adha ya maji kwa zaidi ya wananchi elfu hamsini wa kata nne na vijiji viwili na vitongoji vitatu, mradi utakaokwenda na teknolojia mpya kulipia maji kabla ya kutumia.    

Kikao kazi hicho, kimewakutanisha wadau wote wanaoshiriki katika utekelezaji wa mradi wa maji wa vijiji vitano uliojumuisha, wadau wa kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi cha Nelson Mandela, Tumaini Jipya-New Hope, shirika la WaterAid na eWater kwa kujuisha watalamu wa ngazi ya halmashauri, vijiji na kata, viongozi wawakilishi wa jamii wa kata za nne za eneo la mradi za Lemanyata, Olkokola, Olmotonyi na Olturumet.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.