• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WA ENGALAONI WAKERWA NA MSONGAMANO WA WANAFUNZI DARASANI WAAMUA KUJENGA MADARASA MATATU

Posted on: August 16th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.
      Wananchi wa kijiji cha Engalaoni kata ya Mwandet, halmashauri ya Arusha, wameamua kuunganisha nguvu pamoja na kuanza ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Engalaoni, baada ya kukerwa na adha wanayoipata watoto wao ya kujazana kwnye vyumba vya madarasa wakati wa masomo.

       Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alipotembelea shuleni hapo, Mwenyekiti wa Kamati ya shule, Christopher Laiser, amesema kuwa Wananchi hao wa kijiji cha Engalaoni, wameamua kuanza ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa lwa lengo la kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani kutokana na ongezeko la idadi kubwa ya  wanafunzi linalotokana na Elimu bila Malipo.
      Amefafanua kuwa hamasa ya ujenzi huo wa vyumba vya madarasa, umekuja baada ya serikali kutoa elimu bila malipo, hali ambayo imeondoa vikwazo kwa wazazi wengi na kulazimika kupeleka watoto shule pamoja na  wananchi kuanza kupata mwamko wa kuwapeleka watoto wao shule.

      "Ujenzi huo wa vyumba 3 vya madarasa, umeanza mapema mwezi wa Juni na umefikia hatua ya kupaua sasa, ujenzi  utagharimu shilingi milioni 37 kila darasa likigharimu shilingi milioni 13 kwa kila darasa, mpaka kukamilika kwake" amesema Mwenyekiti huyo.

      Ili kukamilisha ujenzi huo, wananchi wa Engalaoni wanachangia kiasi cha shilingi elfu 42 kwa kila mkuu wa kaya ambaye ni mwanaume pamoja na nguvu kazi kwa wananchi wote, na tayari vifaa vya kukamilisha ujenzi huo vimekwisha nunuliwa viko stoo, tayari kwa ukamilshaji wa jengo hilo kabla ya mwezi Oktoba.

       Naye Mwalimu mkuu shule ya msingi Engalaoni, mwalimu Ester Kimaro, licha ya kuwashukuru na kuawapongeza wananchi wa kijiji hicha, ameeleza  kuwa, ujenzi huo wa vyumba hivyo vya madarasa, utapunguza msongamano wa wanafunzi darasani kwa kiasi, kutokana na shule hiyo kuwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa.
    " Shule ina hii ina jumla ya wanafunzi 1,283 ikiwa na vyumba 9 vya madarasa, idadi inayolazimu zaidi ya wanafunzi 100 kukaa kwenye chumba kimoja cha darasa, hali iliyosababaishwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaoandikishwa shuleni hapo, tangu serikali kutekeleza sera ya elimu bila". Amesema mwalimu Ester.
     Hata hivyo mipango ya wananchi wa Engalaoni kabla ya mwaka huu kumalizika ni kujenga  vyumba vingine viwili vya madarasa pamoja na nyumba za walimu, kutokana na walimu wengi kukosa mahali pa kuishi katika maeneo hayo yasiyo na nyumba za kupangisha.
     Halmashauri ya Arusha inatoa kongole kwa wananachi wa Engalaoni kwa mchango wao mkubwa kwenye sekta ya Elimu, zaidi  inawahamasisha wadau wa  elimu kutoka  mashirika, taasisi na makampuni binafisi, kujitokeza kuchangia na kuwaunga mkono wananchi wa engalaoni kwa ajili ya mtoto wa kitanzania.


PICHA ZA VYUMBA VYA MADARASA S/M ENGALAONI







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.