• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAFUGAJI ARUSHA DC WATAKIWA KUTUMIA MAJOSHO KUOGESHA MIFUGO KWA UFUGAJI BORA NA WENYE TIJA

Posted on: May 7th, 2022

Na. Elinipa Lupembe

Wafugaji Halmashauri ya Arusha, wametakiwa kutumia majosho, kuogesha mifugo yao, ili kuwa na mifugo yenye afya bora, mifugo ambayo itakuwa na tija na kuwaongezea kipato sambamba na kupandisha hali ya uchumi wa familia na Taifa.

Rai hiyo imetolewa na mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, wakati akizindua josho la Kanda C, lililofanyiwa ukarabati na wafugaji wa katika kijiji cha Lemanda kata ya Oldonyosambu, mara baada ya serikali kuanzisha mkakati wa kutoa dawa za kuogeshea mifugo kwa wafugaji.

Mkurugenzi Msumi, licha ya kuwapongeza wafugaji hao kwa kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita, na kuona umuhimu wa kufanya ukarabati wa josho hilo, ili kuikinga na vifo vinavyotokana na magonjwa yanayoenezwa na wadudu aina ya kupe na ndorobo, magonjwa ambayo yanauwa mifigo kwa zaidi ya asilimia 70 mpaka 100, amewataka wafugaji hao kufanya ufugaji wenye tija kwa kuogesha mifugo pamoja na kuipatia chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali.

"Niwatake wafugaji, kuacha kufuga kwa mazoea, fugeni mifugo michache yenye tija, fugeni kwa kiasi, mifugo ambayo mtaweza kuihudumia kwa kuipa chanjo na kuiogesha, ili mifugo hiyo iweze kuwaingizia kipato, tumieni josho hili, kuogesha mifugo yenu, kama watalamu wa mifugo wanavyowaelekeza, hakikisheni mnakuwa na ng'ombe bora, mtakawapeleka sokoni na kuuza kwa bei nzuri" amesisitiza Mkurugenzi Msumi.

Hata hivyo wafugaji hao wa kijiji cha Lemanda, wameishukuru serikali kupitia Wizara ya Mifugo, kwa kuwapatia ruzuku ya dawa ya kuogeshea mifugo, dawa ambayo imewasukuma kukarabati josho hilo, josho ambalo liliacha kutumika zaidi ya miaka 20, kutokana na kushindwa kujiendesha.

Mwenyekiti wa kamati ya kusimamia uendeshaji wa josho la Kanda C, Peter Leskari amesema kuwa, kuzinduliwa kwa josho hilo, kutarudisha matumaini kwa wafugaji, matumaini ambayo yalipotea kwa muda mrefu, ambapo wafugaji walipoteza mifugo yao kutokana na vifo vilivyotokana na magonjwa yanayotokana na kupe na ndorobo na kuahidi kusimamia uendeshaji wa josho hilo ili liwanufaishe wafugaji wote wa eneo hilo.

"Josho hili linatupa uhakika wafugaji wa kuwa na mifugo yenye afya bora, wafugaji wengi walishindwa kumudu gharama kubwa za kuogesha mifugo nyumbani, ng'ombe wengi walikufa na kuzorotesha uchumi wa wafugaji, kupitia josho hili, tumerudisha matumaini kwa wafugaji sasa" ameweka wazi Mwenyekiti huyo wa kamati ya Josho.

Naye Afisa Mifugo halmashauri ya Arusha, Omary Sembe, amefafanua kuwa, serikali kupitia wizara ya mifugo, inatekeleza mkakati wa kuboresha sekta ya mifugo na wafugaji, kwa kutoa dawa za kuogeshea mifugo bure, ili kuzuia vifo vinavyotokana na magonjwa ya kupe na ndorobo, magonjwa ambayo yanaua mifugo kwa zaidi ya asilimia 90.

"Dawa hii ya kuogeshea mifugo, inauwezo wa kuikinga mifugo kwa zaidi ya asilimia 70 ya magonjwa yanayotokana na kupe na ndorobo, ikiwemo magonjwa ya ndigana kali, ndigana baridi, moyo kujaa maj, .....hivyo kuogesha mifugo, kutaondoa vifo vya mifugo visivyo vya lazima" amefafanua Afisa Mifugo.

Awali josho hilo la Kanda C, limekarabatiwa na wafugaji wa kijiji cha Lemanda kwa kushirikiana na halmashauri, kwa gharama ya shilingi milioni 2.8, baada ya srikali kutoa lita elfu 15 za dawa ya kuogeshea mifugo, josho  linategema kuogesha jumla mifugo elfu 90,  ng'ombe elfu 15,  kondooo elfu 42 na mbuzi elfu 33.


Arusha DC

Kazi Inaendelea✍✍✍

 

Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri yaArusha, Seleman Msumi, akichanganya dawa ya kuogeshea mifugo, tayari kwa uzinduzi wa josho la Kanda C, kijiji cha Lemamnda kata ya Oldonyosambu.

Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri yaArusha, Seleman Msumi, akimimina dawa ya kuogeshea mifugo, kwenye josho la Kanda C, kijiji cha Lemamnda kata ya Oldonyosambu, ikiwa ni ishara ya kuzindua josho hilo.

Zoezi la uogeshaji mifugo, limeanza rasmi, mara baada ya uzinduzi wa josho la Kanda C, kijiji cha Lemanda.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.