• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAFUGAJI WAKIRI TEKNOLOJIA YA UHIMILISHAJI KUWAFIKISHA KWENYE KILIMO BIASHARA*

Posted on: August 6th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wafugaji halmashauri ya Arusha, wakiri kunufaika na teknolojia ya uhimilishaji wa ng'ombe, teknolojia  iliyoongeza uzalishaji wa mazao yatokanayo na ng'ombe, mazao yaliyoongeza kipato cha wakulima na kuwapeleka kwenye kilimo biashara.

Wafugaji hao wakiwa wameleta mifugo yao kwenye maonesho ya nanenane Kanda ya Kaskazini, yanayoendelea kwenye viwanja vya Themi - Njiro jijini Arusha, wamekiri teknolojia ya kupandisha ng'ombe kupita chupa ilemeta mapinduzi makubwa katika uzalishaji na ongezeko la mazao ya mifugo.

Abraham Abraham, mfugaji kutoka kitongoji cha Ilkiushi , kata ya Olturumet, amekiri matumizi ya teknolojia ya uhimilishaji imeleta mapinduzi makubwa kwa wafugaji, kwa kuwapatia ng'ombe bora, wanaokua haraka huku wakizalisha maziwa na nyama nyingi zaidi tofauti na hapo awali walipokuwa wanafuga ng'ombe wa asili.

Amefafanua kuwa wafugaji kwa sasa, wanajivunia teknolojia hiyo, na kumuelezea ng'ombe wake anayeitwa Spika  mwenye umri wa miezi 20, ana uzito wa kilo 600 na tayari ana mimba ya miezi 6, mwenye uwezo wa kutoa lita 30 mpaka 35 za maziwa kwa siku, maziwa ambayo yakiuzwa yatampatia kiasi cha shilingi elfu 49 kwa siku.

"Ngombe huyu ni mtamba ambaye amepatikana kwa kutumia teknolojia ya Uhimilishaji, ni mchanganyiko wa mbegu za  fresian na asian, amesajiliwa kwa namba  0001642, mwenye uwezo wa kutoa maziwa lita 30 -35 kwa siku, huku maziwa hayo yakiingiza takribani shilingi milioni 17.6 kwa mwaka" Amebainisha mfugaji  Abraham

Naye Alfayo Mollel, mfugaji na msindikaji wa bidhaa za maziwa, amebainisha kuwa teknolojia ya uhimilishaji imewapa matumaini wafugaji, na kuongeza kuwa kwa sasa mradi wake wa ufagaji ng'ombe, unajiendesha wenyewe kupitia maziwa yake na kuleta faida kubwa tofauti na ufugaji wa zamani ambapo ng'ombe alitoa lita 3 za maziwa kwa siku.

"Teknolojia hii imeleta matumaini kwetu wafugaji, upatikanaji wa maziwa mengi umeniwezesha kuanzisha kiwanda cha kusindika maziwa na kuliongezea thamani zao la maziwa, kwa sasa ninapark maziwa fresh, mtindi, yoghot, samli na siagi, pamoja na matumizi ya gesi ya kinyesi 'bio gas' ambayo pia nimeanza kuuza kwa majirani zangu" Amefafanua Alfayo

Naye Daktari wa  Mifugo halmashauri ya Arusha Dkt. Yohana Kiwone, amethibitisha ubora wa teknolojia ya uhimilishaji na upatikanaji wa ngombe bora wenye kuleta faida kubwa kwa wafugaji, ngombe ambao wanauwezo wa kutoa maziwa mengi, nyama nyingi,ngozi bora pamoja na kinyesi kinachotoa gesi kwa matumizi ya nyumbani na mwisho hutumika kama mbolea kwa kilimo.

Dkt. Kiwone amewasisitiza wafugaji kubadilika na kufanya kilimo biashara kwa kufuga mifugo michache kwenye eneo dogo huku wakitumia teknolojia za kisasa ya uhimilishaji pamoja na kuwatumia watalamu wa mifugo ili kupata mazao bora na kufikia Ajenda ya 10 -30 ya Kilimo biashara.


KAULI MBIU: AJENDA YA 10 -30 KILIMO NI BIASHARA 'SHIRIKI KUHESABIWA KWA MIPANGO BORA YA KILIMO


PICHA ZA MATUKIO KWENYE BANDA LA MIFUGO 

Mfugaji Abraham Abraham kwenye banda la Mifugo la Halmashauri ya Arusha  akionesha ng'ombe aliyezaliwa kupitia  teknolojia ya Uhimilishaji ya kupandikizwa mbegu zilizotokana na ng'ombe wa aina mbili tofauti, wakati wa maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini kwenye viwanja vya Themi Njiro.



Ng'ombe wa nyama kwenye banda la Mifugo la Halmashauri ya Arusha, aliyezaliwa kupitia  teknolojia ya Uhimilishaji ya kupandikizwa mbegu zilizotokana na ng'ombe wa aina mbili tofauti, wakati wa maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini kwenye viwanja vya Themi Njiro.


Dkt. Yohana Kiwone akiwa kwenye banda la Mifugo la Halmashauri ya Arusha  akionesha teknolojia ya Uhimilishaji namna mbegu zinavyohifadhiwa na kupandikizwa kwa ng'ombe, wakati wa maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini kwenye viwanja vya Themi Njiro.


Mfugaji Alfayo Mollel, akionesha kifaa rahisi cha kuondoa mafuta 'cream' kwenye maziwa ikiwa ni mchakato wa  kusindika maziwa, kwenye Maonyesho ya Nanenae Kanda ya Kaskazini.

Mfugaji Alfayo Mollel, akionesha kifaa rahisi cha kutengeneza samli, kwenye Maonyesho ya Nanenae Kanda ya Kaskazini eneo la Themi Njiro

D

Daktari wa Mifugo Dkt. Linus (aliyevaa kofia) kitoa maelekezo kwa mteja aliyetembelea banda la Mifugo kupitia picha,  juu ya magonjwa ya mifugo na namna ya kukabiliana nayo, wakati wa maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini yanayoendelea kwenye viwanja vya Themi Njiro

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.