Na Elinipa Lupembe
Wafugaji halmashauri ya Arusha, wakiri kunufaika na teknolojia ya uhimilishaji wa ng'ombe, teknolojia iliyoongeza uzalishaji wa mazao yatokanayo na ng'ombe, mazao yaliyoongeza kipato cha wakulima na kuwapeleka kwenye kilimo biashara.
Wafugaji hao wakiwa wameleta mifugo yao kwenye maonesho ya nanenane Kanda ya Kaskazini, yanayoendelea kwenye viwanja vya Themi - Njiro jijini Arusha, wamekiri teknolojia ya kupandisha ng'ombe kupita chupa ilemeta mapinduzi makubwa katika uzalishaji na ongezeko la mazao ya mifugo.
Abraham Abraham, mfugaji kutoka kitongoji cha Ilkiushi , kata ya Olturumet, amekiri matumizi ya teknolojia ya uhimilishaji imeleta mapinduzi makubwa kwa wafugaji, kwa kuwapatia ng'ombe bora, wanaokua haraka huku wakizalisha maziwa na nyama nyingi zaidi tofauti na hapo awali walipokuwa wanafuga ng'ombe wa asili.
Amefafanua kuwa wafugaji kwa sasa, wanajivunia teknolojia hiyo, na kumuelezea ng'ombe wake anayeitwa Spika mwenye umri wa miezi 20, ana uzito wa kilo 600 na tayari ana mimba ya miezi 6, mwenye uwezo wa kutoa lita 30 mpaka 35 za maziwa kwa siku, maziwa ambayo yakiuzwa yatampatia kiasi cha shilingi elfu 49 kwa siku.
"Ngombe huyu ni mtamba ambaye amepatikana kwa kutumia teknolojia ya Uhimilishaji, ni mchanganyiko wa mbegu za fresian na asian, amesajiliwa kwa namba 0001642, mwenye uwezo wa kutoa maziwa lita 30 -35 kwa siku, huku maziwa hayo yakiingiza takribani shilingi milioni 17.6 kwa mwaka" Amebainisha mfugaji Abraham
Naye Alfayo Mollel, mfugaji na msindikaji wa bidhaa za maziwa, amebainisha kuwa teknolojia ya uhimilishaji imewapa matumaini wafugaji, na kuongeza kuwa kwa sasa mradi wake wa ufagaji ng'ombe, unajiendesha wenyewe kupitia maziwa yake na kuleta faida kubwa tofauti na ufugaji wa zamani ambapo ng'ombe alitoa lita 3 za maziwa kwa siku.
"Teknolojia hii imeleta matumaini kwetu wafugaji, upatikanaji wa maziwa mengi umeniwezesha kuanzisha kiwanda cha kusindika maziwa na kuliongezea thamani zao la maziwa, kwa sasa ninapark maziwa fresh, mtindi, yoghot, samli na siagi, pamoja na matumizi ya gesi ya kinyesi 'bio gas' ambayo pia nimeanza kuuza kwa majirani zangu" Amefafanua Alfayo
Naye Daktari wa Mifugo halmashauri ya Arusha Dkt. Yohana Kiwone, amethibitisha ubora wa teknolojia ya uhimilishaji na upatikanaji wa ngombe bora wenye kuleta faida kubwa kwa wafugaji, ngombe ambao wanauwezo wa kutoa maziwa mengi, nyama nyingi,ngozi bora pamoja na kinyesi kinachotoa gesi kwa matumizi ya nyumbani na mwisho hutumika kama mbolea kwa kilimo.
Dkt. Kiwone amewasisitiza wafugaji kubadilika na kufanya kilimo biashara kwa kufuga mifugo michache kwenye eneo dogo huku wakitumia teknolojia za kisasa ya uhimilishaji pamoja na kuwatumia watalamu wa mifugo ili kupata mazao bora na kufikia Ajenda ya 10 -30 ya Kilimo biashara.
KAULI MBIU: AJENDA YA 10 -30 KILIMO NI BIASHARA 'SHIRIKI KUHESABIWA KWA MIPANGO BORA YA KILIMO
PICHA ZA MATUKIO KWENYE BANDA LA MIFUGO
Mfugaji Abraham Abraham kwenye banda la Mifugo la Halmashauri ya Arusha akionesha ng'ombe aliyezaliwa kupitia teknolojia ya Uhimilishaji ya kupandikizwa mbegu zilizotokana na ng'ombe wa aina mbili tofauti, wakati wa maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini kwenye viwanja vya Themi Njiro.
Ng'ombe wa nyama kwenye banda la Mifugo la Halmashauri ya Arusha, aliyezaliwa kupitia teknolojia ya Uhimilishaji ya kupandikizwa mbegu zilizotokana na ng'ombe wa aina mbili tofauti, wakati wa maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini kwenye viwanja vya Themi Njiro.
Dkt. Yohana Kiwone akiwa kwenye banda la Mifugo la Halmashauri ya Arusha akionesha teknolojia ya Uhimilishaji namna mbegu zinavyohifadhiwa na kupandikizwa kwa ng'ombe, wakati wa maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini kwenye viwanja vya Themi Njiro.
Mfugaji Alfayo Mollel, akionesha kifaa rahisi cha kuondoa mafuta 'cream' kwenye maziwa ikiwa ni mchakato wa kusindika maziwa, kwenye Maonyesho ya Nanenae Kanda ya Kaskazini.
Mfugaji Alfayo Mollel, akionesha kifaa rahisi cha kutengeneza samli, kwenye Maonyesho ya Nanenae Kanda ya Kaskazini eneo la Themi Njiro
D
Daktari wa Mifugo Dkt. Linus (aliyevaa kofia) kitoa maelekezo kwa mteja aliyetembelea banda la Mifugo kupitia picha, juu ya magonjwa ya mifugo na namna ya kukabiliana nayo, wakati wa maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini yanayoendelea kwenye viwanja vya Themi Njiro
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.