Mahakama ya Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha imewahukumu wanaume wawili kifungo cha Maisha kwa kosa la kumbaka na kumlawiti mtoto mwenye umri wa miaka nane mkazi wa kijiji Emaoi kata ya Olmotony, halmashauri ya Arusha.
Wanaume hao ni Bw. Michael Lukas (52) na Bw. Gabriel Ambrose (33) ambao ni wakazi pia wa kijiji cha Emaoi, baada ya kukutwa na hatia ya kutenda makosa hayo kwa nyakati tofauti.
Katika kesi hiyo ambayo imeendeshwa na mahamiku wawili kwa nyakati tofauti, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya wilaya, Mhe. Gwantwa Mwankuga na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya Mhe. Nguvava waliwatia hatiani wanaume hao wwawilina kuwahukumu kifungo cha Maisha jela baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa pasipo na shaka yoyote.
Mtuhumiwa wa kwanza Gabriel Ambrose (33)alitiwa hatiani na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya Mhe. Nguvava mapema Mei 30 mwaka huu kwa kosa hilo huku mtuhumiwa wa pili akiwasomewa hukumu yake leo Juni 09, 2023 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya wilaya, Mhe. Mwankuga.
Aidha, imeelezwa kuwa mtoto huyo alibakwa na kulawitiwa na wanaume hao mwezi Februari mwaka huu nyumbani kwao ambapo anaishi na baba yake baada ya mama yake mzazi kufariki mwaka 2020 ambapo mtuhumiwa wa kwanza Bw. Ambrose alitumia fursa hiyo kumfuata mtoto huyo ndani ya nyumba yao wanayoishi kumbaka na kumlawiti wakati baba akiwa ameenda kwenye majukumu yake ya kila siku.
Mtuhumiwa wa pili Bw. Michael Lukas alikuwa akimtuma mtoto huyo dukani kununua vitu na wakati akirejea anamdanganya na kumuingiza ndani kwake kumbaka na kumlawiti.
Hata hivyo, mahakama baada ya kujiridhisha na Ushahidi imeamua kutoa adhabu hiyo kali kwa watuhumiwa wote kwa makosa hayo ili iwe ni fundisho kwa watu wengine wenye nia ovu ya kutaka kufanya vitendo kama hivyo kwa watoto.
Kwa upande wake Mdau kutoka dawati la haki ya mama na mtoto BAKWATA Farida Moseneka, licha ya kuishukuru Mahakama hiyo pamoja na Serikali kwa kutenda haki dhidi ya mtoto huyo, Ameiomba jamii kuendelea kutoa ushirikiano kwa kuibua matukio ya kikatili yanayotendeka kwenye jamii na kuyafikisha kwenye uongozi wa Serikali kwaajili ya kuyachukulia hatua za kisheria badala ya kusuluhisha kimila na kupelekea mtoto kukosa haki yake ya msingi.
Naye Afisa Ustawi wa Jamii Kiongozi halmashauri ya Arusha, Beatrice Tengi ameipongeza mahakama kwa kutenda haki kwa kuhakikisha haki ya mtoto imepatikana
Ameongeza kuwa licha ya kuwa serikali kwa kushirikiana na wadau inatoa elimu kwa kwa jamii juu haki za watoto, bado kuna changamoto kwa jamii kufanya ukatili kwa watoto na baadhi ya wanajamii kushindwa kutoa ushahidi kwenye kesi kwa kuhofia kutengwa na ndugu, jamaa na marafiki.
ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.