Na Elinipa Lupembe
Wajumbe wa Kamati ya fedha Utawala na Mipango, halmashauri ya Arusha, wakikagua mradi wa ujenzi wa nyumba ya mtumishi cha Zahanati ya Loovilukuny, kata ya Kisongo.
Mradi huo wa nyumba ya mtumishi umekamilika na umegharimu kiasi cha shilingi milioni 50, fedha kutoka Serikali Kuu, ikiwa ni utekelezaji wa malengo ya Serikali ya kuboresha na kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya nchini hususani kwa wananchi waishio vijijini.
Ziara hiyo ya kikazi ya kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ni ya kawaida kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za uendeshaji wa serikali za Mitaa kwa kuzingatia Utawala Bora wa uwazi na uwajibikaji.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.