• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAJUMBE WA MTAKUWWA ARUSHA DC,  WAIOMBA HALMASHAURI KUTOA ENEO LA KUJENGA NYUMBA SALAMA.

Posted on: March 23rd, 2022

Na. Elinipa Lupembe

Wajumbe wa Kamati ya kupinga Ukatili dhidi ya Watoto na Wanawake halmsahauri ya Arusha wameiomba halmashauri hiyo, kutoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kuwatunzia watoto waliofanyiwa vitendo vya ukatili, maarufu kama Nyumba Salama.

Wajumbe hao wamefikia maamuzi ya kufikisha ombi hilo kwa Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, baada ya kukutana na changamoto ya mahali pa kuwatunza watoto walipota madhila ya kufanyiwa vitendo vya ukatili, azimio lililofikiwa wakati wa kikao maalum cha kamati hiyo kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Kijiji cha Watoto SOS - Ngaramtoni.

Wajumbe hao wamebainisha changamoto hiyo ya muda mrefu, ya halmashauri hiyo kukosa kituo cha kudumu cha Nyumba Salama, kwa ajili ya kuwahifadhi na kuwatunza watoto wenye mgogoro wa kisheria, wakati kesi zao zinaaendelea kusikilizwa, imesababisha baadhi ya kesi kupoteza uhalisia na ushahidi na hatimaye watuhumiwa kuachiwa huru.

"Halmashauri ya Arusha haina kituo maalum kwa ajili ya kuhifadhi watoto, waliofanyiwa vitendo vya ukatili, tunalazimika kuwaapeleka kwenye kituo kilichopo Jiji la Arusha, jambo ambalo kituo kile kinaelemewa na idadi kubwa ya watoto, hivyo ni vema halmashauri ya Arusha ikawa na Nyumba salama yake" amefafanua Afisa Jinsia Rovil Nguyaine

Hata hivyo wajumbe hao wamebainisa umuhimu wa Nyumba Salama ni kutokana na ukweli kwamba, tafiti zinaonesha watoto wengi hufanyiwa vitendo vya ukatili na watu walio ndani ya familia ndani na jamii zao, jambo ambalo linaonekana  endapo mtoto atafanyiwa ukatili na tukio hilo kupelekwa kwenye vyombo vya sheria, kuendelea kukaa kwenye familia au jamii iliyomtendea ukatili huo, ni rahisi mtoto huyo kushawishika na kupoteza ushahidi wa kesi husika.

Mwaansheri wa Halmashuri ya Arusha, Eliasifiwe Kileo, amebainisha kuwa, ni hatari sana mtoto, aliyefanyiwa ukatili kuendelea kuishi kwenye familia au jamii iliyomfanyia ukatili, jambo ambalo huzuia kupatikana kwa ushahidi halisi wa kesi hiyo sambamba na kupoteza haki ya mtoto husika.

"Mtoto aliyefanyiwa vitendo vya ukatili, akiendelea kukaa kwenye familia au jamii, iliyomfanyia ukatili huo, mara nyingi ushahidi wa kesi hizo huharibiwa kwa mtoto kurubuniwa au kushawishiwa na familia, ili kuharibu ushahidi, jambo ambalo humkosesha mtoto, haki yake ya msingi kisheria" amesisiituza Mwanasheri huyo

Naye Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya Arusha na Afisa Mifugo Wilaya Omary Sembe, amekiri kutambua umuhimu wa kituo hicho na kuahidi kufikisha jambo hilo kwenye menejimenti ili litafutiwe ufumbuzi wa haraka, kutokana na umuhimu wake, na hatimaye halmashauri ya Arusha kuwa Nyumba Salama, kama ilivyo takwa na agizo la Serikali kwa maslahi ya watoto na Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo baadhi ya Wadau wa masuala ya watoto na wanawake, ambao ni wajumbe wa Kamati hiyo, wameweka wazi kuwa, kutokana na umuhimu wa kituo hicho, endapo halmashauri itatoa eneo kwa ajili ya ujenzi, watakuwa tayari kushiriki ujenzi wa Nyumba hiyo salama.

.ARUSHA DC 4

KaziInaendelea✍✍✍










Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.