• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAJUMBE WA MTAKUWWA ARUSHA DC WATAKIWA KUBUNI MBINU THABITI KUKABILIANA NA ONGEZEKO LA UKATILI WA KIJINSIA

Posted on: July 14th, 2022

Na Mwandishi wetu.

Kamati ya Mpango Mkakati wa Kupambana na Kutokomeza Ukatili halmashauri ya Arusha (MTAKUWWA), imetakiwa kubuni mbinu mpya za kukabiliana na ukatili wa kijinsia ili kupunguza ongezeko la vitendo vya kikatili wa kijinsia vinavyotendeka katika jamii.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha ambaye ni mwenyekiti wa kamati MTAKUWA halmashauri hiyo, Seleman Msumi, katika mafunzo yanayoendelea kutolewa kwa wanachama wa kamati ya MTAKUWWA yaliyofanyika katika ukumbi wa chama cha walimu Tanzania.

Mkurugenzi Msumi amefafanua kuwa suala la ukatili wa kijinsia ni mtambuka hivyo Serikali yenyewe haiwezi kumaliza tatizo hilo bila kushirikiana na asasi zisizo za kiserikali ili kuifikia jamii kwa urahisi zaidi kwa kuwa matukio ya ukatili wa kijinsia yanaleta madhara makubwa katika kizazi kijacho.“Ni imani yangu kuwa asasi zisizo za kiserikali kwa kushirikiana na Serikali zikifanya kazi kwa kushirikiana zitaleta mabadiliko chanya na kuisadia jamii kuepukana na ukatili wa kijinsia”. Amesisitiza Msumi.

Naye mwezeshaji wa mfunzo hayo, Philbert Mashingia ameweka wazi kuwa, mabadiliko yanaanza na mtu mmoja mmoja hivyo ni jukumu la kila mzazi kujitathimini na kama yeye mwenyewe ndiye chanzo cha kusababisha ukatili wa kijinsia badala ya kuitupia lawama jamii inayomzunguka.

Aidha wa Pamoja na wadau walioshiriki katika mafunzo hayo wamebainisha baadhi ya sababu zinazopelekea ongezeko la ukatili wa kijinsia, ni pamoja na mila na desturi zilizopitwa na wakati kama vile ukeketaji na ndoa za utotoni na kuwataka wazazi kuonyesha ushirikiano ili kutokomeza vitendo hivyo vya kikatili. 

“Kuna changamoto kama vile suala la rushwa lakini tutajitahidi baada ya mafunzo haya kuendelea kutoa elimu kwa mtu mmoja mmoja ili jamii ipate uelewa juu ya madhara ya ukatili wa kijinsia kwani wahanga wakubwa ni watoto na wanawake”. Amesema Joseph Piniel, mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo. 

Hata hivyo, Afisa Maendelo ya jamii halmashauri ya Arusha, Angela Mvaa amesema kuwa, kwa sasa jamii inapata taarifa kuhusu ukatili wa kijinsia na wako tayari kuonyesha ushirikiano kwa kuibua zaidi matukio ambayo yalikuwa yanafumbiwa macho hapo awali.  Mafunzo ya wajumbe wa MTAKUWA yanatolea na shirika la Shalom Center na kushirikiana na shirika la UZIKWASA, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wajumbe hao kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuifikia jamii na kutokomeza ukatili wa kijinsia. 


ARUSHA DC

KaziIendekee ✍✍

JIANDAE KUHESABIWA

PICHA MBALIMBALI ZA MATUKIO

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya MTAKUWWA Seleman Msumi, akitoa mchango wake wakati wa mafunzo yanayoendelea kutolewa kwa wanachama wa kamati hiyo kuhusu namna ya kukabiliana na Ukatili wa kijinsia


Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi akiwa na wanakamati wengine kwenye majadiliano katika makundi


Mwezeshaji wa mafunzo ya Ukatili wa kijinsia, Philbert Mashingia akitoa mafunzo kwa wanakamati wa MTAKUWWA





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.