Na Elinipa Lupembe.
Katika mkakati wa kutekeleza Ajenda 10 - 30 Kilimo Biashara, wakulima wametakiwa kufanya tafiti kwenye soko kabla ya kuotesha mazao, lengo likiwa kufahamu mazao yanayohitajika sokoni kwa msimu husika ndipo wajipange kulima zao ambalo litauzika kwa bei nzuri wakati wa mavuno kulingana na msimu.
Kwa kuanza kufanya tafiti sokoni kutamuwezesha mkulima kufikia Ajenda 10 - 30 ya Kilimo biashara kwa kulima kulingana na mahitaji ya mazao yanayohitajika sokoni na kuuza kwa bei ambayo itampatia faida kubwa.
Watalamu wa Kilimo halmashauri ya Arusha, wamebainisha kuwa wanaendelea na mkakati wa kutoa elimu kwa wakulima, kabla ya kuotesha zao flani, ni vema kufanya tafiti kwenye masoko, ili kutambua mahitaji ya zao katika soko kwa wakati husika ndipo arudi shambani kulima zao ambalo linahitajika sokoni kwa wakati huo.
Afisa Kilimo mbogamboga, halmashauri ya Arusha, Lucy Mvungi, ameweka wazi kuwa, wakulima wamekuwa wakilima kwa mazoea bila kufanya tafiti za uhitaji wa soko kwa wakati huo, matokeo yake inapofikia kipindi cha mavuno, huuza mazao kwa bei ndogo na kujikuta wakipata hasara tofauti na matarajio yao.
"wakulima wengi wanalima kwa mazoea, wakiona mmoja analima nyanya wote watajielekeza kulima nyanya, jambo ambalo ikifikia kipindi cha mavuno nyanya zinafurika na zinakosa bei, inamlzimu mkulima kuuza kwa bei ya chini sana na kujikuta napata hasara na weakati mwingi hukata tamaa ya kuendelea na kilimo, hivyo utafiti kwa mkulima nijambo la muhimu sana na lifanyike katika hatua ya mwanzo kabisa wakati wa maandalizi ya kulima" Amesistiza Lucy
Ameongeza kuwa, Ili kuondoakana na changamoto hiyo, wakulima wanashauriwa kuanzia sokoni kutambua uhitaji wa soko, ndipo kurudi shambani kufanya kilimo kulingana na hitaji la soko kwa wakati husika.
baada ya kuamua zao la Kulima, Aidha Afisa Kilimo huyo amesisitiza pia uchaguzi wa mbegu bora ni muhimu katika kilimo ili kupata mazao bora na mengi kwa ajili ya kupata faida na kuongeza kipato zaidi.
Inashauriwa mkulima kutumia mbegu ambazo zimeandaliwa kitaalamu ili kupata mavuno bora na kwa wingi kuliko kurudia kupanda mbegu mara baada ya kuvuna zao husika.
Maonesho ya Nanenane 2022 kanda ya Kaskazini yanendelea kwenye viwanja vya Nanenane eneo la Themi - Njiro Jijini Arusha yenye Kaulimbiu ya "AJENDA YA 10 -30 KILIMO NI BIASHARA 'SHIRIKI KUHESABIWA KWA MIPANGO BORA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI"
SHIRIKI SENSA YAWATU NA MAKAZI 2022.
JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022
PICHA ZA MATUKIO
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.