• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI NA MAAFISA ELIMU KATA WATAKIWA KUSIMAMIA VIGEZO 12 VYA USIMAMIZI WA TAALUMA SHULENI...

Posted on: February 8th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Wasimamizi wa shule ikiwemo wakuu wa shule za sekondari na Maafisa Elimu kata wametakiwa kusimamia vigezo 12 vya usimamizi wa taaluma shuleni, ili kufikia lengo la serikali la kuketa matokeo chanya na makubwa kwenye elimu ya sekondari nchini.


Rai hiyo imetolewa na kaimu Mkurugenzi halmashauri ya Arusha, Elizabeth Ngobei, lengo likiwa kufiki vigezo ambavyo vimetolewa na serikali kupitia ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kuhakikisha kila kigezo kinafanyiwa kazi na kupimwa utekelezaji wake kila miezi mitatu ya robo ya mwaka.


Aidha amewataka wasimamizi hao wa elimu kuendelea kusimamia utoaji wa elimu kwa kuzingatia vigezo vilivyoainishwa kwenye mkataba kazi kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni ili kujiweka kwenye nafazi nzuri katika utendaji kazi.


"Mkataba  huu unavyo vigezo 12 vya kuzingatia kuanzia ngazi ya Taifa na kila ngazi ina majukumu yake lakini watendaji wakubwa ni ninyi walimu na wanafunzi, fanyeni tahmini ya utendaji kama ilivyoelekezwa zaidi hakikisheni mnaiwezesha  halmashauri kufikia malengo hayo ya serikali". Amesisitiza Kaim Mkurugenzi.


Naye Mkuu wa Idara ya Elimu sekondari, halmashauri ya Arusha Mwl. Menard Lupenza, amevitaja vigezo hivyo 12 kuwa, ni pamoja na kusimamia utoaji wa taaluma kwa kuboresha ufundishaji na ujifunzaji, kuhakikisha wanafunzi wote waliopangiwa kidato cha kwanza wanaripoti shuleni.


Kudhibiti utoro na kupunguza mdondoko wa wanafunzi, kusimamia utoaji wa chakula shuleni hasa kwa shule za kutwa, kuboresha matokeo ya mitihani ya ndani na ile ya Taifa kwa kuondoa alama F na kufanya tahmini ya matokeo pamoja na kuainisha changamoto, kuhakikisha wanafunzi wanajifunza na kuijua lugha ya kiingereza.


Ameongeza kuwa wakuu wa shule wanawajibu wa kuhakikisha masomo yote yanafundishwa kwa ufasaha huku walimu mahiri wakifundisha kidato cha kwanza, pamoja na kuwalinda watoto dhidi ya vitendo viovu vya ukatili na udhalilishaji.


Aidha ameahidi kuwasimamia watendaji wote walio chini yake  kwa kuhakikisha kila mmoja anatekeleza wajibu wake pamoja na kuhakikisha walimu wanapata stahiki zao pamoja na mafunzo kazini huku akisisitiza kuwachukulia hatua wale watakao kwenda kinyume au kukwamisha utekelzaji wa vigezo vilivyoainishwa kwa namna yoyote.


Hata hivyo wasimamizi hao wa elimu ngazi ya shule na kata, wamebainisha kuwa vigezo vilivyoanishwa vikifanyiwa kazi vina tija kwa kuwa vinaondoa kasumba ya utendaji kazi wa mazoea na kuwawezesha kufanya kazi  kwa weledi, ubunifu na kwa uwanda mkubwa.


Mkuu wa shule Kiranyi, Mwl. amesema kuwa  vigezo vilivyoainishwa una tija kubwa ukiwa umegusa maslahi ya mwalimu na wanafunzi na kuongeza kuwa walimu kwa sasa wanaenda kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia vigezo vya upimaji, vigezo ambavyo vitamlazimu mwalimu kuwajibika ili kufikia malengo.


Awali wakuu wa shule za sekondari halmashauri ya Arusha pamoja na Maafisa Elimu wa kata zote wamesaini mkataba wa kazi wa kusimamia Elimu, zoezi lililoambatana na kikao cha tathmini ya matokeo ya mtihani wa Taifa ya kidato cha nne mwaka 2022.


ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

#KaziInaendelea✍
















Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.