Na Elinipa Lupembe
Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini, mradi unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF awamu ya IV, wametakiwa kutimiza masharti ya msingi ya ruzuku ya fedha wanazozipokea ili kuimarisha sifa za kuwa kwenye mpango.
Akizungumza wakati wa zoezi la ugawaji ruzuku ya fefha kwa mwezi wa 7/8, 2022, Mratibu wa TASAF halmashauri ya Arusha, Grace Makema, amesema kuwa, TASAF inatoa fedha hizo kwa walengwa zikiwa na masharti ya kutimiza, ili mlengwa aendelee kuwa na sifa za kupokea ruzuku hiyo.
Amewataka walengwa hao kuzingatia masharti hayo, ikiwa ni pamoja na masharti ya afya kwa kaya zenye watoto wa kuanzia miaka 0-5, kwa kuhakikisha watoto hao, wanahudhuria kliniki kwa kipindi chote, pamoja na kupata chanjo zote stahiki kwa miaka hiyo mitano.
Ameongeza kuwa, kaya pia zinatakiwa kuzingatia masharti ya elimu, kwa kaya zenye watoto wa miaka 6-18, kuhakikisha wanakwenda shule na kuhudhuria masomo ya kwa siku zote bila kukosa huku wakiwapatia watoto hao mahitaji muhimu ya shule.
"TASAF imeandaa utaratibu wa kufanya Warsha za Jamii, ili kutoa mafunzo kwa walegwa kila wakati wa zoezi la kugawa ruzuku, hivyo tunasisitiza kila mlengwa kuhudhuria warsha za jamii, ili kuendelea kupata ufahamu zaidi wa huduma zinazotolewa na mpango, haki, wajibu na umuhimu wa kutimiza masharti ya ruzuku" . Amefafanua Mratibu Grace.
Hata hivyo walengwa wa kijiji cha Laroi, wamepongeza, serikali kupitia TASAF kwa kuziwezesha kaya zao kiuchumi, huku wakiendelea kupewa elimu ya matumizi ya fedha na kutambua haki na wajibu wao kama wanufaika wa mpango huo,
Mwenyekiti wa kijiji cha Laroi, Mhe. Remingi Joseph, amebainisha kuwa uwepo wa program mbalimbali za mafunzo kwa walengwa unasaidia walengwa na jamii kupata uelewa wa pamoja juu ya miradi ya TASAF na ruzuku za fedha wanazopokea walengwa.
"Mradi wa TASAF licha ya kuwainua kiuchumim lakini pia umewafanya wananchi kuchangamsha akili na kubadilika kifikra kwa kuwa wanajumuika na wenzao kwenye vikundi na miradi lakini zaidi wanapata mafunzo yanayowawezesha kubadilika na kukua kifikra" Ameweka wazi mhe. Remigi
Awali katika dirisha la mwezi wa 7/8, jumla ya shilingi milioni 617.1, zimetolewa kwa kaya 12,288 katika vijiji 88 vya halmashauri ya Arusha, huku kaya hizo zikipokea fedha kwa njia ya mitandao ya simu, benki, mawala na fedha tasmu.
ARUSHA DC,
TUPO KAZINI.
Mwenyekiti wa kijiji cha Laroi, Mhe. Remigi Joseph, akiwahudumia walengwa wa mpango wa Kunusuru kaya masikini waliofika kupokea ruzuku ya malipo ya mwezi 7/0 2022, kwenye ofisi ya kijiji hicho.
Afisa Mtendaji wa kijiji cha Laroi, Saning'o Moiyo, (aliyeshikamkaratasi) akisoma majina ya wanakaya mpango wa Kunusuru kaya masikini waliofika kupokea ruzuku ya malipo ya mwezi 7/0 2022, kwenye ofisi ya kijiji hicho.
Mwenyekiti wa kijiji cha Lemanda, Mhe. Moses Kalombo, akiwahudumia walengwa wa mpango wa Kunusuru kaya masikini waliofika kupokea ruzuku ya malipo ya mwezi 7/0 2022, kwenye ofisi ya kijiji hicho.
Wanakaya wa kijiji cha Laroi, wakisubiri taratibu za malipo ya ruzuku ya malipo ya mwezi 7/0 2022, kwenye ofisi ya kijiji hicho.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.