• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WALIMU ARUSHA DC WAKABIDHIWA VISHIKWAMBI

Posted on: January 7th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Walimu 1,442 wa shule za msingi na sekondari halmashauri ya Arusha wamekabidhiwa vishikwambi, ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya serikali yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa

Akikabidhi vishikwambi hivyo, Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango amewataka walimu  kutumia nyenzo hizo muhimu za kidijitali kwa lengo lililokusudiwa ikiwa ni pamoja na kupandisha kiwango cha taaluma shuleni.

"Seikali imeona umumimu wa walimu kupatiwa vitendea kazi vya kidigitali ili kurahisisha tendo la kufundisha na kujifunzia, walimu mnalo jukumu la kuvitumia kulingana na maelekezo pamoja na kuvitunza  ili kufikia lengo la serikali". Amesisitiza Mhandisi Ruyango

Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi amesema kuwa vishikwambi hivyo vinapaswa kutumiwa kwa mujibu wa miongozo ya Serikali ni mali ya Umma na vitasimamiwa kwa mujibu wa sheria ya manunuzi ya Umma na kanuni zake.

Ameongeza kuwa mwalimu anatakuwa kutumia vishikwambi hivyo kwa ajili ya kupata matini ya masomo, vitabu rejea pamoja na picha za video zinazohusu masomo na si vinginevyo.

Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Mwl. Salvatory Alute licha ya kuishukuru serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na mama Samia Suluhu, ameahidi kusimamia matumizi na utunzaji wa vishikwambi hivyo, na kuhakikisha vinatumika kupandisha taaluma shuleni na kufikia lengo la serikali.

"Tunaamini matumizi ya teknolojia rahisi shuleni, yanakwenda kufanya mapinduzi ya kitaaluma kwa kumuwezesha mwalimu kupata maarifa na ujuzi ikiwemo matini ya masomo, mbinu za kufundishia na kujifunzia kuendana na mabadiliko ya Sayansi na teknolojia". Amebainisha Afisa Elimu Mkuu  Mwl. Alute


Hata hivyo walimu hawakusita kumshukuru mhe. Rais Samia Suluhu, kwa kuona umuhimu wa walimu kuwa na kitendea kinachowatoa kwenye analojia na kuwapeleka kwenye dijitali.

Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Lesiraa, Mwl. Dora Ngobei amethibitisha kuwa vishikwambi hivyo ni nyenzo muhimu na rahisi itakayomuwezesha mwalimu, kupata na kuhifadhi matini ya masomo, pamoja na vitabu rejea vitakavyomjenga kuwa na maarifa mapya kila wakati.

"Hiki ni kitendea kazi muhimu kwa mwalimu, licha ya kupunguza gharama ya matumizi ya karatasi, kitasaidia pia ujazaji wa taarifa kwenye mifumo, ambapo awali ilikuwa ngumu kwa shule ambazo hazikuwa na kompyuta". Amesema Mkuu wa shule sekondari Likamba Mw. Richard Mugyabuso

Awali Mkuu huyo wa wilaya amekabidhi vishkwambi hivyo kwa wakuu wa shule za sekondari, walimu wakuu wa shule za msingi pamoja na maafisa elimu wa kata zote kwa niaba ya walimu wote, zoezi lililofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri hiyo.


ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍






















Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.