• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAFUNZI WASICHANA SHULE YA SEKONDARI LOSINONI JUU, WAIOMBA SERIKALI KUWAJENGEA MABWENI

Posted on: March 31st, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Wanafunzi wa kike shule ya sekondari Losinoni kata ya Oldonyowas, wameiomba serikali kuwajengea bweni ili waweze kulala shuleni, kutokana na changamoto inayowakabili ya kutembea umbali mrefu, kwenda na kurudi shuleni kila siku.

Wananafunzi hao wametoa rai hiyo, kupitia shairi waliloliimba mbele ya mgeni rasmi, wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa kutoka kwa wadau wa maendeleo wa shule hiyo, hafla iliyofanyika shuleni hapo, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Kupitia shairi hilo, wanafunzi hao, licha ya kuwashukuru wadau kwa misaada wanayoitoa kwenye shule hiyo, misaada ambayo inachochea maendeleo ya shule pamoja na wanafunzi kitaaluma, lakini walienda mbali zaidi na kuiomba serikali na wadau kuwajengea mabweni kwa kuwa asilimia kubwa ya wanafunzi hao, wanaishi umbali mrefu kutoka shuleni hapo.

"Tunashukuru kwa misaada mingi inayotolewa na serikali na wadau, tunaomba mtufikirie zaidi, wenzenu tunatembea mpaka Kilomita 24, kwenda na kurudi shuleni, hili linakatisha ndoto za watoto wengi wa Losinoni, kwa baadhi yetu kuamua kuacha shule kwa kukata tamaa, na wakati mwingine wasichana huamua kuolewa, serikali yetu tunaomba mtusaidie ili watoto wa Losinoni nao wasome na kutimiza ndoto zao kama watoto wengine wa kitanzania" Walitoa ujumbe huo kupitia beti ya shairi lao

Wanafunzi hao, waliendelea kufafanua kwa hisia kubwa kuwa, wakati mwingine wanafunzi hunusurika kushambuliwa na wanyama wakali, kutokana na vijiji vyao kupitiwa na Korido ya wanyama pori, wanaotembea kati ya Hifadhi za  Taifa za Arusha na Manyara na kuongeza kuwa, shule imezungukwa pia na makorongo makubwa, hivyo kipindi cha mvua inakuwa tatizo kwa wanafunzi kwenda na kurudi shuleni. 

Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, alipokea ujembe huo kwa hisia sana, na kuahidi kufanyia kazi suala hilo, huku akiwaomba wadau wa maendeleo kujitokeza kuchangia ujenzi wa mabweni shule hiyo ya sekondari Losinoni.

"Watoto wangu, mmenipa ujembe huu, kwa hisia kali sana, mimi kama mzazi, nimelipokea tatizo na ninaahidi kwenda kulifanyia kazi kwa haraka ili tupate mabweni katika shule yenu na muweze kusoma na kutimiza ndoto zenu, niwapongeze kwa shairi lenu ambalo limebeba ujumbe mzito sana, kwa maslahi ya watoto wa kitanzania na Taifa kwa ujumla". Amesisistiza Mkurugenzi Msumi.

Shuel ya Sekondari ya Losinoni ni miongozpniwa mwa shuke za kata ilianzisjwa kwa nguvu za wananchi wa Kijiji cha Losinoni kwa ushirikiano na Hifadhi ya Taifa Arusha ANAPA, pamoja na halamshauri ya Arusha, na kuanza rasmi kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka mwaka 2016, 





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.