• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAFUNZI SEKONDARI MRINGA WAISHUKURU SERIKALI UJENZI NA UKARABATI WA MABWENI....

Posted on: September 1st, 2023

Na Elinipa Lupembe

Wanafunzi wa shule ya sekondari Mringa, halmashauri ya Arusha wameishukuru serikali kwa kuwajengea abweni mapya pamoja na kukarabati mabweni ya zamani yaliyokuwa yamechakaa shuleni hapo, ujenzi  unagharimu kiasi Cha shilling million 360 fedha kutoka serikali kuu kupitia mradi wa SEQUIP.


Wakizungumza na mwandishi wetu, wanafunzi shuleni hapo, wameeleza furaha waliyonayo kutokana na kuongezewa mabweni mapya na kukarabatiwa yale ya zamani kuwa, uwepo wa mabweni hayo licha ya kuwa na sehemu bora ya kulala itaongeza ari ya kusoma na kuongeza ufaulu wao, usalama wa wanafunzi na mali zao, kuondoa utoro pamoja na kuondoa hofu waliyokuwa nayo ya kuambukizana magonjwa kutokana na msongamano na kuwafanya kuishi kwa nafasi sasa.


Christine Mkama mwanafunzi wa kidato cha sita ameishukuru serikali ya mama Samia kwa kujenga mabweni hayo ambayo wa amekiri kuamini kuwa mabweni hayo, yatawawezesha wanafunzi kuishi kwa nafasi kulingana na idadi yao pamoja na kuongeza ari ya kusoma na ufaulu pia.


 "Tunaishukuru serikali, tunamshukuru mama  Samia kwa kuendelea kutujali wanafunzi hasa wasichana na kuona umuhimu wa kutujengea mabweni mapya, mabweni pamoja na usimamizi mzuri wa walimu yanatupa hamasa ya kusoma vizuri na kufaulu mitihani yetu" Amesema Christine.


Kiongozi wa Serikali ya Wanafunzi Grace John,  amebainisha kuwa na upungu wa mabweni shuleni hapo, uliosababisha baadhi ya wanafunzi kuwa na ufaulu wa chini, na kuongeza kuwa mapinduzi yaliyofanywa na serikali ya mama Samia, yatawapa  nafasi nzuri ya kujisomea na kuweza kufaulu zaidi.


Naye Mkuu wa shule ya sekondari Mringa Mwl. Salim Magaka, amesema kuwa shule ilipokea shilingi milioni 360, milioni 260 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili huku million 100 zikiwa ni za ukarabati wa mabweni manne na matundu ya vyoo, mabweni ambayo yalikuwa yamechakaa sana kutokana na kujengwa kwa miaka mingi iliyopita.


"Mabweni haya yote ni kwaajili ya wanafunzi wa kike na kukamilika kwake tunategemea kupunguza msongamano mabwenini na utakaochochea ari ya wanafunzi kujisomea  na kuwezesha ufaulu kuongezeka". Mwl. Magaka


Awali Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu halmashauri ya Arusha,  Anna urio ameongeza kuwa halmashauri ya Arusha imepokea shilingi  bilioni 1.4 fedha za mradi wa SEQUIP kwa ajili ya kutekeleza miradi elimu sekondari na kufafanua kuwa milioni 360, ujenzi na ukarabati wa mabweni shule ya sekondari Mringa, milioni 580.3 ujenzi wa shule mpya ya sekondari Moivo na milioni    ikiwa ni ujenzi wa nyumba ya walimu shule ya sekondari Kiutu


"Tunatemea kukamilika kwa miradi yote, kutafikia lengo la serikali la kuboresha miundo mbinu ya shule nchini la kuwezesha mazingira bora ya kujifunzia, kuwezesha idadi kubwa ya watoto wa kitanzania kupata fursa ya elimu na kutimiza ndoto zao za kielimu hata kuwafikia watoto ambao wazazi wao hawakuwa na na uwezo wa kuwasomesha watoto wao" Amesema Anna.


Ujenzi na ukarabati wa miradi hiyo unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Oktoba 2023.


ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA✍

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.