• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI ARUMERU WATAKIWA KUTUMIA TEHAMA KWA MAENDELEO YA TAIFA

Posted on: June 19th, 2021

Na Elinipa Lupembe.

Kiongozi wa mbio Mbio za Mwenge Maalum wa Uhuru 2021 Kitaifa, Luteni Josephine Paul Mwambashi, amewataka wananchi wa Arumeru, kuacha kutumina vibaya, teknolojia ya Habari na mawasiliano TEHAMA, badala yake kuitumia vema teknoljia ambayo ina kasi kubwa ya katika kuharakisha  maendeleo ya mtu binafsi na  Taifa kwa ujumla.

Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge Kitaifa, amesema hayo, wakati akitoa ujembe wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru 2021, zilipotembelea na kukagua jumla ya miradi tisa ya maendeleo katika wilaya ya Arumeru, yenye halmashauri mbili za Arusha na Meru.

Ameweka wazi kuwa, kutokana na mabadiliko ya Sayansi na Teknoloji duniani sasa, TEHAMA ikitumika vizuri, inauwezo mkubwa wa kuleta maendeleo katika sekta zote muhimu, huku akiwasisitiza vijana, kujikita kujifunza matumizi ya teknolojia hiyo ya mawasiliano, teknolojia ambayo dunia imejielekeza huko.

TEHAMA inarahisisha kufanyika kwa kazi mbalimbali ikiwemo ukusanyaji wa mapato, na kuzitaka halamshauri kukusnaya mapato kwa kutumia mashine, huku akiwasisitiza wafanya biashara kutumia mashine za EFD, na kuwakumbusha wananchi kuhakikisha wanachukua risiti pindi wanapofanya manunuzi.

Hata hivyo Kiongozi huyo wa Mwenge wa Uhuru kitaifa, licha ya kuwataka wananchi kutumia TEHAMA kwa maendeleo, amewasistiza pia wananchi kujihadhari na vitendo vya rushwa, kwa kuwa rushwa ni kinyume na haki za binadamu na inarudisha nyuma maendeleo.na kuongeza kuwa afya ya kila mtu ni muhimu hivyo kujikinga na magonjwa ya Malaria na UKIMWI.

Aidha Kiongozi huo wa Mwenge wa Uhuru kitaifa Lutwn Josephine, hakuacha kuwasisistiza wananchi, kujali afya zao kwa kuzingatia lishe bora, lishe amabayo inawafanya wananchi kuwa na afya bora kwa ajili ya ujenzi wa taifa la Tanzania.

Mwenge wa UHURU 2021 umekimbizwa umbali wa Kilomita 126.3 katika halmashauri  zote mbili, kutembelea jumla ya miradi tisa (9) yenye thamani ya shilingi Bilioni 2.3 katika sekta ya Afya, Elimu, Maji, Barabara na Uwekezaji.

Mwenge huo Maalumu wa Uhuru 2012, umefanya shughuli za kuzindua mradi wa TEHAMA shule ya msingi Mlangarini, mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya sekondari Kikwe na mradi wa jengo la mama na mtoto hospitali ya wilaya ya Olturumeti na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa  mradi barabara Sangisi - Nambala, mradi wa kusukuma maji Losikito pamoja na mradi wa Kituo cha Mafuta Africa Petrol kata ya Oloirieni.

Aidha Mwenge Maalum wa Uhuru 2021, umetembelea na kukagua mradi wa shamba la migomba na tumbaku kata ya Olturumeti, miundombinu ya wanafunzi wenye mahitaji maalum shule ya msingi Ilboru na kukamilsha kwa kutembelea mradi wa Kikundi cha vijana -Umoja Youth Group kata ya Moivo.

Kauli  Mbiu ya Mwenge wa Uhuru 2021 “TEHAMA ni Msingi wa Taifa endelevu; itumie kwa usahihi na Uwajibikaji”.










Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.