• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI ARUSHA DC WAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA MAZINGIRA DUNIANI...

Posted on: September 27th, 2023

Wananchi halmashauri ya Arusha wameshiriki maadhimisho ya Siku ya Afya ya Mazingira Duniani, kwa kufanya usafi maalum kwenye maeneo yao, huku kilele cha maadhimisho hayo kikifanyika kwenye kata ya Olmotonyi.


Wananchi hao wamefanya usafi kwenye maeneo yanayowazunguka pamoja na maeneo ya wazi huku wakiiomba Serikali kutilia mkazo suala la Usafi ili kudumisha afya za wananchi kwa Maafisa Afya kutembelea wananchi kila wakati na kutoa elimu juu ya umuhimu wa kufanya usafi kwenye maeneo yao.


Akizungumza mmoja wa wananchi hao wakati wa zoezi hilo la usafi, Linda Hagai ambaye ni mhudumu wa mgahawa, amesema kuwa siku hiyo ni muhimu sana kwaajili ya kuhamasisha wananchi kujiwekea tamaduni za kudumisha usafi kwenye maeneo yanayowazunguka ndani na nje.


"Tunaiomba serikali iendelee kututembea na kuhamasisha suala la usafi ili kila mwanachi awe na uelewa juu ya suala hili na sio tu kufanya hivyo wakati wa maadhimisho ya siku hii". Amesisitiza Linda.


Adinan Msangi aliyeshika kandarasi ya kukusanya  taka ngumu eneo la Olmotony, amesema kuwa,wananchi wameadhimisha siku hiyo kwa kufanya usafi wa maeneo ma kuongeza kuwa kila mara wamekuwa wakiwahasisha wananchi kusafisha mazingira yao pamoja na kuhakikisha wanahifadhi taka vizuri mpaka hapo zitakapochukuliwa na magari ya taka.


Hata hivyo Afisa wa Afya halmashauri ya Arusha, Issa Msumari ametoa rai kwa wananchi wote wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanafanya usafi wa mazingira kila wakati pamoja na kuweka misingi thabiti ya matumizi sahihi ya vyoo, unawaji mikono baada ya kutoka chooni, uhifadhi na utupaji wa taka ulisahihi ili kuboresha afya ya Jamii na kuepukana na magonjwa ya mlipuko.


"Kupitia siku hii muhimu, tunawahamasisha wananchi wote ndani ya halmashauri yetu kuhakikisha kwamba wanazingatia vigezo na misingi yote ya afya ili tuweze kuboresha afya ya jamii na kuepukana na magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu". Amesema Afisa Afya huyo.


Ameongeza kuwa halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na wadau wa afya, jeshi la polisi na wanachi wamefanya usafi wa kuzunguka maeneo ya kata ya Olmotony na vitongoji vyake huku kila mmoja akitakiwa kuzingatia kanuni mbalimbali za afya ili kujinga na magonjwa ya mlipuko yatokanayo na uchafu


Siku ya Afya ya Mazingira Duniani imeasisiwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa lengo la kutoa fursa ya kuchukua hatua na kuhamasisha jamii kuhusu masuala yanayohusiana na afya ya mazingira huku masuala ya uchafuzi wa hewa, maji na udongo, matumizi ya kemikali hatari, uchafuzi wa mazingira vijijini na mijini, kuhifadhi bioanuwai, mabadiliko ya tabianchi, usafi wa mazingira na utawala bora wa mazingira yakitiliwa mkazo na huadhimishwa mwezi Septemba kila mmwaka


ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA

#KaziIendelee✍


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.