• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI KIJIJI CHA LEMANDA WAMSHUKURU MAMA SAMIA UJENZI WA SHULE MPYA. YA MSINGI

Posted on: June 5th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Wananchi wa kijiji cha Lemanda kata ya Oldongosambu wamemshukuru Mhe. Rais mama Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa mradi wa ujenzi wa shule mpya ya msingi kijijini kwao.

Wakizungumza mbele ya Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, kwenye eneo la mradi huo, wamesema kuwa uwepo wa shule kijijini hapo, utawapa fursa watoto wao kupata elimu na kutimiza ndoto zao, tofauti na hapo awali ambapo watoto wengi hawakusoma na wasichana kuolewa kwenye umri mdogo.

Wamesema kuwa kutokana na ukubwa wa kijiji na kata hiyo yenye shule mbili za msingi, watoto hulazimika kutembea umnali wa zaidi ya Km 18 mpaka 20 kwenda na kurudi shuleni, jambo ambalo lilikatisha tamaa watoto wengi na kuamua kuacha shule na wengi kutokufanya vizuri kwenye mitihani yao huku watoto wadogo wakiandikishwa shule kwa kuchelewa kwa kuhofia umbali huo.

Faraja Charles (27) Mama wa watoto watatu  ametuma salamu za shukrani kwa mama Samia, kwa kuwajali kinamama wa Lemanda kwa kusogeza shule kijijini kwao, jambo ambalo lilikuwa ni ndoto, huku wakiamini watoto wao kupata elimu kama ilivyo watoto wengine wa kitanzania.

Kiongozi wa mila wa ukoo wa Lukumai, Laigwanani Saringe Naromosha, amesema kuwa wameona serikali inafanya kazi, walikuwa na njaa ikawaletea  mahindi na muda mfupi akaleta pesa za kujenga shule.

"Sisi tulidhani serikali itapambana na njaa tuu, lakini punde si punde imeleta mradi wa shule, tunamshukuru sana mama Samia na tunamuombea kwa Mungu, aongoze vizuri kwa kuwajali wananchi wa hali ya chini" Amethibitisha Laigwanani huyo.

Diwani wa kata ya Oldonyosambu, Raymond Rairumbe,  amemshukuru Mhe. Rais kupitia mradi huo wa fedha nyingi kijijini hapo, mradi ambao unakwenda kuwahudumia watoto wa familia za wafugaji ambao wengi walikosa fursa hiyo tangu kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika 

"Kiukweli tumeshuhudia serikali ya awamu ya sita ikifanya kazi, kata hii imepata zaidi ya 45% ya fedha zote za mradi wa BOOST zilizoletwa halmashauri ya Arusha, tumepata milioni 306 .9  kati ya milioni 682.5, kiasi ambacho ni kikubwa ukilinganisha na fedha zilizokwenda maeneo mengine, tunathibitisha mama yuko kazini, Nani kama mama" Ameweka wazi Mhe. Diwani huyo.

Shule mpya ya msingi, inajengwa kwa gahrama ya shilingi milioni 306.9 ikijumuisha ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa ya awali, vyumba 7 vya madarasa ya msingi, matundu 16 ya vyoo pamoja na jengo la utawala.

Awali, jumla ya shilingi milioni 682.5 kutoka Serikali Kuu kupitia Mradi wa Kuboresha Upatikanaji wa Fursa sawa katika Ujifunzaji Bora kwa Elimu ya Awali na Msingi Tanzania Bara (BOOST), fedha zitakazotumika katika ujenzi wa miundombinu ya shule 6 za Awali na Msingi.

Ikumbukwe kuwa, miradi hiyo ya ujenzi wa miundombinu shule za msingi ni utekelezaji wa Ilani ya CCM, Sura ya tatu Ibara ya 79 kifungu (q)Kukarabati miundombinu ya kufundishia na kujifunzia na kifungu (C)Kuboresha uratibu na usimamiaji wa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu.

ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.