• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI KIJIJI CHA LOSINONI JUU WAPATA MWAROBAINI WA VIFO VYA MAMA NA MTOTO

Posted on: October 9th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Wananchi wa kijiji cha Losinoni Juu kata ya Oldonyowas, halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, wamepata utatuzi wa changamoto ya Vifo vya kinamama na watoto wakati wa kujifungua, vilivyosababishwa na ukosefu wa  Zahanati katika kijiji hicho kwa miaka nenda rudi.


Changamoto hiyo imepata ufumbuzi wa kudumu, mara baada ya shirika la Friends of Tanzania - ARUSHA, kwa kupitia ufadhili wa wananchi wa nchini Ujerumani, kukamilisha ujenzi wa  zahanati ya Losinoni Juu  na kuikabidhi kwa Serikali ya Kijiji cha Losinoni Juu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi na kukabidhi Zahanati hiyo, Mratibu wa mradi shirika la Friends in Tanzania -ARUSHA, Harald Pfiffer, amesema kuwa, wananchi wa Ujerumani walitambua changamoto za huduma za afya,  zilizokuwa zikiwakabili wananchi wa Losinoni Juu, na kuona umuhimu wa kuwajengea Zahanati hiyo ili kuokoa maisha ya wananchi wa eneo hilo.


Pfiffer ameongeza kuwa, licha ya yeye kuwa rafiki wa wananchi wa Losinoni Juu, kwa muda mrefu sasa, lakini ameridhishwa zaidi na uongozi wa Rais John Pombe Magufuli wa kuwahudumia wananchi hasa wa vijijini, maeneo ambayo kuna changamoto nyingi za kijamii na kuwataka wananchi hao kukitumia kituo hicho pamoja na kutunza jengo hilo.


Naye mgeni rasmi na mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amelishukuru shirika hilo, kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano, na kuwaomba wadau hao kuendelea kusaidia ujenzi wa nyumba za watumishi ili huduma hiyo, iweze kutolewa kwa saa 24 na siku saba za wiki.

Aidha mkuu wa Wilaya huyo, amewataka wananchi wa kijiji hicho, kutumia Zahanati hiyo, na kuwasisitiza kina mama wajawazito kuhudhuria Kiliniki muda wote wa ujauzito,  kuacha tabia ya kujifungulia nyumbani pamoja na kuwapeleka watoto wa umri wa chini ya miaka mitano kupata chanjo zote zinazostahili.

Ameongeza kuwa, lengo la serikali ya awamu ya tano, ni kupunguza na kutokomeza vifo vya mama na mtoto, kwa kusogeza huduma za afya kwa wananchi, kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na Zahanati,  kata kuwa na kituo cha Afya pamoja na hospital za Wilaya na mikoa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya.

"Serikali ya awamu ya tano, inashirikiana na wadau wa ndani na nje ya nchi, kutokomeza vifo vya mama na mtoto, tunahakikisha kila huduma zinapatikana kuanzia ngazi ya kijiji kuwe na Zahanati, kila kata iwe na kituo cha afya, hospitali za wilaya na za mkoa" amesisitiza mkuu huyo wa wilaya.


Mheshimiwa Muro, amefafanua kuwa, serikali itahakikisha kuleta watumishi watakaotoa huduma katika Zahanati hiyo,, gari la kubrbea wagonjwa, na kuwataka wananchi kujiunga na mfuko wa BIMA ya Afya Iliyoboreshwa kwa gharama ya shilingi elfu 30 tu, ili kupata dawa na vifaa tiba katika zahanati hiyo.


Hata hivyo, wananchi wa kijiji cha Losinoni Juu, wamedhihirisha kufurahishwa na ujenzi wa Zahanati hiyo, na kuthibitisha kuwa changamoto ya vifo vya mama na mtoto vinavyosababishwa na ukosefu wa huduma za afya kwa karibu sasa imefikia kikomo, na kukiri kutumia zahanati hiyo kwa ajili ya kuokoa maisha yao.


 Mama Sara, mkazi wa kijiji cha Losinoni Juu, amesema kuwa, kinamama wajawazito wamekuwa wakitembea umbali mrefu kupata huduma za kliniki na kujifungua, jambo ambalo lilisababisha, wajawazito kujifungulia njiani na wengine kupoteza maisha  huku wazazi wengi wakishindwa kuwapeleka watoto wao kliniki kwa utaratibu uliopangwa.


"Kutokana na umbali, wazazi wengi hawawapeleki watoto kliniki, wajawazito hushindwa kuhudhuria kliniki, wengi kujifungulia nyumbani, na inapotokea tatizo la kupekwa hospitali hujifungulia njiani na wengine kupoteza maisha ya mama na mtoto" amethibitisha mama Sara.

Zahanati hiyo imejengwa kwa gharama ya shilingi milioni 56 na kufanya halmashauri ya Arusha kufikisha jumla ya Zahanati 48, Vituo vya afya 7 na hospitali 2, lengo kubwa likiwa ni upatikanaji wa huduma na afya pamoja na dawa zote za msingi, ili kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.