Na. Elinipa Lupembe.
Wanannzengo wa mtaa wa Ikigiji eneo la Boswelu Manispaa ya Ilemela, wamejitokeza kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Arusha,marehemu Richard Kwitega, kwenye makazi yake yaliyoko eneo la Boswelo, Manispaa ya Ilemela, Jijini Mwanza.
Katika kutoa salamu za mwisho, Wannzengo hao wamemuelezea marehemu Kwitega, kuwa alikuwa mtu wa tofauti sana, na jirani mwema kwao, licha ya kipindi kifupi walichoishi naye, katika Nnzengo hiyo ya Ikigiji.
Akitoa salamu za pole mbele ya mamia ya waombolezaji, waliofika kwenye makazi ya marehemu Kwitega, Mwenyekiti wa huduma za Jamii, Nnzengo ya Ikigijo, Christopher Kilasa, amemuelezea marehemu akwitega kuwa kwa muda mfupi walioishi naye walimfahamu kwa ushiriki wake katika masuala ya kijamii licha ya kuishi eneo hilo kwa muda mfupi.
"Marehemu alikuwa jirani yetu mwema, asiye na makuu, wengi hawakujipambanua na cheo chake, bali aliheshimu kila mtu wa Nnzengo hii bila kujali uwezo wake kiuchumi, hakuwa mbinafsi bali alikuwa ni mkarimu, mwenye upendo aliyeshirikiana na majirani kila aliopofika katika Nnzengo ya Ikigiji" amesimulia Mwenyekiti huyo wa Nnzengo ya Ikigijo
Hata hiyo wananchi hao waliweka wazi hisia zao za majonzi, mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, mheshimiwa Idd Kimanta, kuelezea namna kifo cha marehemu Kwitega kilivyotokea, akiwa safarini kutekeleza majukumu yake ya kazi, na kumuelezea namna alivyokuwa mchapakazi na mwenye kujituma katika kazi huku akiwa na ushirikiano mkubwa na wafanyakazi wenzie bila kujali nafasi zao
Awali marehemu Richard Kwitega, alifariki kwa ajali ya gari, iliyotokea eneo la Mdolii - Babati mkoani Manyara, akiwa safarini kuelekea mkoani Dodoma kikazi.
PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO, NYUMBANI KWA MAREHEMU KWITEGA
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.