• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAWAKE KAYA ZENYE UHITAJI ILKINDING'A WAMSHUKURU MAMA SAMIA KUPEWA MRADI WA MBUZI WA MAZIWA KUPITIA TASAF

Posted on: February 27th, 2023

Na Elinipa Lupembe.

Wanawake walio kwenye mpango wa Kunusu kaya masikini kijiji cha Ilkiding'a,  wameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mh. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa mtaji wa mbuzi wa maziwa kupitia Mfuko wa maendeleo ya Jamii - TASAF III awamu ya  II kwa ufadhili wa OPEC IV.


Wanawake hao, wameishukuru serikali wakati wakikabidhiwa mbuzi wa maziwa kwa ajili ya kufuga na kujiongezea kipato, zoezi lililofanyika kwenye viwanja vya ofisi ya kijiji hicho.



Wamesema kuwa serikali imezijali kaya masikini, licha ya kuwapatia fedha za ruzuku lakini imeweza kuwapa mradi wa  mbuzi wa maziwa,  chakula cha kuanzia,  mafunzo ya kitalamu pamoja na chanjo na kuahidi kuwatunza mbuzi hao vizuri ili waweze kuzaa na kuleta mafanikio kwenye familia zao.


Sara Lobulu (88) ameweka hisia zake kwa kumshukuru mama Samia kwa kuwakumbuka wanawake wazee na wajane, mradi ambao amekiri utakwenda kuwasaidia wanakaya hao kukuza kipato na kuweza kutunza familia.


"Tunaishukuru serikali, tunamshukuru mama Samia,  ametusaidia sisi wanawake wenzake, ametambua namna tunaelemewa katika kutunza familia zetu, ameona ni vizuri kutusaidia kupunguza makali ya maisha". Amesema mama Sara


Elinita Rogathe mama wa watoto 4, naye licha ya kuishukuru serikali kupitia TASAF kwa kuweziwezesha kaya masikini  kupata mtaji wa mbuzi wa maziwa, mradi ambao wanaamini utazinufaisha kaya zao na kuziinua kiuchumi na kuahidi kutunza vizuri mbuzi hao ili waweze kuzaliana na kuongezeka.


Naye Diwani wa kata ya Ikiding'a Mhe. Francis Lukumai amemshukuru Mhe. Rais, Samia Suluhu kwa kuwawezesha wananchi wa hali ya chini kujikwamua kutoka kwenye lindi la umaskini na kuwataka wanakaya hao kutumi fursa hiyo vizuri ili kukuza pato la kaya.


Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amewasihi wanavikundi hao kutunza mbuzi hao ili wawawezeshe kujikwamua kiuchumi, na kuongeza kuwa Serikali inatambua hali duni za wananchi wake na kuja na mkakati wa kuwawezesha kujikwamua kiuchumi kupifia miradi ya TASAF.


"Leo tumekabidhi mbuzi 80 tunategemea tukirudi kukagua mradi tutakukuta wamezaliana mara mbili, hakikisheni mtaji huu unakua na kujikwamua kiuchumi, tusiwauze wala kuwachinja, mbuzi hawa ni wa maziwa nendeni mkahakikishe baada ya muda kila mwanakaya anakuwa na idadi kubwa ya mbuzi ili kufikia malengo ya serikali". Amesema Mkurugenzi Msumi


Awali Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Arusha, Grace Makema, amebainisha kuwa mradi huo uliibuliwa na walengwa hao, na kufanikiwa kukabidhiwa jumla ya mbuzi 80 wenye thamani ya shilingi milioni 22.1 wamekabidhiwa kwa vikundi vitano vyenye wanakikundi 15 sawa na kaya 75 zikinufaika kwa kila kikundi kupata mbuzi wa maziwa 16.


Ametaja kiasi hicho cha fedha kimejumuisha gharama za ununuzi wa mbuzi, mafunzo kwa wanavikundi, chakula cha kuanzia ufugaji, dawa kinga pamoja na ufuatiliaji kwa watalamau wa mifigo, na kuongeza kuwa , wanakaya hao watafuga mbuzi hao wa maziwa chini ya uangalizi wa serikali ya kijiji kupitia Afisa Ugani wa kijiji kwa kuwapatia mbinu bora za ufugaji pamoja na chakula cha kuanzia ufugaji.


Ikumbukwe kuwa, mradi wa TASAF ni miongoni mwa miradi inayotekelezwa na serikali ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi wa kupambana na umaskini nchini.


ARUSHA DC Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

KaziInaendelea✍✍











Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.