• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANUFAIKA WA TASAF WATAKIWA KUTUMIA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA MFUKO HUO KUWANUFAISHA KIJAMII NA KIUCHUMI.

Posted on: March 8th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini halmashauri ya Arusha wametakiwa kuitunza, kuithamini na kuitumia vema miradi ya TASAF ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na Serikali.

Rai hiyo imetolewa na wajumbe wa Kamati ya kusimamia ofisi ya Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakikishi Zanzibar, walipotembelea miradi wa ujenzi wa nyumba ya mtumishi Zahanati ya Likamba, mradi unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), kata ya Musa.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Machano Othman Said, amesema kuwa miradi hiyo ni muhimu kwa maendeleo na maslahi ya jamii nzima kwa kupambana na maadui watatu, ujinga, umasikini na maradhi.

Lengo la serikali kupitia mpango wa uhawilishaji fedha ni kuhakikisha kila kaya inapata mahitaji yake ya msingi huku miradi ya miundombinu ikiwezesha upatikanaji wa huduma za kijamii ndani ya maeneo wanayoishi.

"Tumeshuhudia  miradi ilivyopendeza, wenyewe mmethibitisha umuhimu wa miradi hii kwenu, ni jukumu lenu sasa kuitunza ili idumu vizazi na vizazi lakini zaidi tumieni fursa hii kuibua miradi mingine zaidi" . Amesisitiza Mwenyekiti huyo

Akisoma taarifa ya mradi huo, Afisa Mtendaji wa kijiji,  amesema kuwa mradi wa nyumba ya watumishi wa Afya yenye sehemu mbili (2in 1), umegharimu kiasi cha shilingi milioni 77 fedha kutoka serikalini kupitia TASAF IV OPEC III, unategemewa kuishi familia mbili za wahudumu wa afya wa zahanati hiyo ya Likamba.

Hata hivyo wanufaika wa mpango wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini kijiji cha Musa, wameshukuru TASAF na kutoa shuhuda za namna mpango huo ulivyoleta mapinduzi ya kiuchumi na kijamii ndani ya kijiji chao.

"Tunaishukuru TASAF kwa kutufumbua macho, wanawake tulikuwa gizani, TASAF imetupa mafunzo ya kukabiliana na umasikini, leo tumeweza kukaa kwenye vikundi kuwekeza pesa na kukopeshana, tumeweza kushirikiana na kuanzisha miradi ya kuongeza kipato kwenye kaya zetu, tunaamini TASAF imeletwa na Mungu". Amesema Mary Lemburis

Sanare Sayuni amemshukuru Mhe. Rais Samia, kwa kuwajali wananchi wa hali ya chini, uwepo wa nyumba ya mtumishi kwenye zahanati hiyo, utaondoa vifo visivyo vya lazima vya wanawake na watoto wakati wa kujifungua pamoja na uhakika wa upatikanaji wa huduma za afya kwa saa 24.

Wajumbe hao kutoka  baraza la Wawakilishi  Zanzibar wamefanya ziara ya mafunzo kwa siku tatu mkoani Arusha na kutembelea miradi 4 halmashauri ya Arusha na Meru.


"ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

#kaziinaendelea✍✍✍✍

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.