Na. Elinipa Lupembe
Miaka minne ya awamu ya tano, Serikali imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa wadau wa maendeleo, ikiwa ni pamoja na kushirikiana nao kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta mtambuka.
Halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na mdau Bogarooke East Africa Trust, wamejenga mabweni mawili ya wasichana, shule ya sekondari Olmotony Forest kata ya Olmotony, miundombinu iliyogharimu shilingi milioni 245.
Mabweni hayo yenye kulaza wanafunzi 120, yamewapunguzia wanafunzi wa kike, adha ya kutembea umbali mrefu kwenda na kurudi shuleni, yameongeza ari ya wanafunzi wa kike kujisomea pamoja na kupunguza changamoto ndoa za utotoni, changamoto inayowakabili watoto wa kike, kwa kuwa sasa, wanaishi shuleni, yakiwa ni mazingira salama zaidi kwao.
Halmashauri ya Arusha, inaendelea kuwakaribisha wadau wa ndani na nje ya nchi, kuendelea kujitoa kwa hali na mali kuchangia maendeleo katika sekta ya Elimu, ikiwa ni pamoja na kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli.
#TUMEAMUA#TUNATEKELEZA#
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.