Na.Elinipa Lupembe.
Wasimamizi wa miradi halmashauri ya Arusha, miradi inayotekelezwa na fedha za miradi kutoka serikali Kuu, kwa ajili ya ukamilishaji wa miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2020/2021, wametakiwa kusimamia miradi hiyo kwa weledi na kuhakikisha, inakamilika kwa wakati kwa kuzingatia ubora unaoendana na thamani ya fedha zilizotolewa na serikali.
Rai hiyo imetolewa na Afisa Mipango, halmashauri ya Arusha, Anna Urio, wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua na kufuatilia hali ya utekelezaji wa miradi hiyo, katika sekta ya Afya na Elimu, miradi inayogharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.9.
Afisa Mipango huyo, amefafanua kuwa, licha ya kuwa miradi hiyo, inaendelea vizuri lakini amewasistiza, wasimamizi wa miradi hiyo, kuhakikisha wanafuata kanuni, sheria na taratibu za matumiz ya fedha za serikali huku wakihakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ubora na kwa wakati uliopangwa.
Aidha ameweka wazi kuwa miradi hiyo, inatelelezwa kwa kutumia 'forced account' na kusimamiwa na wakuu wa shule, wasimamizi wa vituo vya Afya pamoja na kamati za ujenzi katika maeneo hayo, na kuongeza kuwa kamati hizo zinatakiwa kufuata kanuni na taratibu zote zilizoainishwa kisheria huku wakihakikisha miradi hiyo inakuwa na uwiano wa majengo na thamani ya pesa walizopokea 'value for. money'
"Kwa wastani kasi ya ujenzi inakwenda vizuri, na miradi imekamilika kwa zaidi ya asilimia 50, hivyo niwatake wasimamizi wa miradi, kukabiliana na chngamoto za kimazigira zinazojitokeza pamoja na kuwahimiza wakandarasi kuongeza kasi ya ujenzi, kwa kuwepo site kila siku, ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kuanza kuwahudumia wananchi" amesisistiza Afisa Mipango huyo.
Hata hivyo wajumbe wa kamati za ujenzi, ambao ni wasimamizi wa miradi hiyo, wamekiri kuendelea kujitolea kusimamia miradi hiyo kwa weledi, hasa kwa kutambua umuhimu wa serikali kuruhusu ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali yao.
Awali timu hiyo ilitembelea na kukagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa jengo la mionzi 'Xray', jengo la mama na mtoto 'RCH' Kituo cha afya Nduruma, ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi, ujenzi wa mabweni 6, ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na vyoo katika shule za sekondari na msingi.
ARUSHA DC
Kazi inaendeleea✍✍✍
PICHA ZA MIRADI
Timu ya ufuatilija utekelezaji wa miradi ya maendeleo, halmashauri ya Arusha, wakizungumza na wajumbe wa Kamati ya ujenzi ya miradi ya miwili ya jengo la mama na mtoto pamoja na ujenzi wa jengo la mionzi 'Xray' kituo cha afya Nduruma.
Mhandisi wa ujenzi halamshauri ya Arusha, Eng. Seleman Kiba akikagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya sekondari Ilkiding'a
Mradi wa ujenzi wa jengo la mama na mtoto kituo cha afya Nduruma
Timu ya ufuatilija utekelezaji wa miradi ya maendeleo halamshauri ya Arusha, ikikagua mradi wa ujenzi wa jengo la mionzi 'Xray' kituo cha afya Nduruma
Vyumba vya madarasa shule ya sekondari Ilkiding'a
Bweni la wavulana shule ya sekondari Einoti
Bweni la wasichana shule ya sekondari Einoti
Vyumba vya madarasa shule ya msingi Kambi ya Maziwa
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.