• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI WA KATA ARUSHA DC WASAINI MKATABA WA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA AFUA ZA LISHE

Posted on: November 3rd, 2022

Na Elinipa Lupembe

Maafisa Watendaji wa kata 27 za halmashauri ya Arusha, wamesaini mkataba wa upangaji, ufuatiliaji na utekelezaji wa shughuli za Lishe kwenye maeneo ya kata zao, huku wakitakiwa kufanya kazi hiyo kwa kuzingatia malengo makuu mawili, viashiria na vigezo tisa vilivyoainishwa kwenye makataba huo.

Maafisa hao wamesaini mkataba huo baina yao na Mkurugezni Mtendaji halmashauri ya Arusha, Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Mganga mkuu pamoja na Mratibu wa Lishe, ikiwa ni hatua ya  muendelezo wa uingiaji wa mikataba ya usimamizi wa shughuli za afua za lishe kuanzia ngazi ya Taifa, Mkoa, wilaya na na hatimaye  ngazi ya kata na  vijiji.

Akizungumza wakati wa zoezi la utiaji saini mikataba  hiyo, Kaimu Mkurugenzi Halmashauti ya Arusha, Elizabeth Ngobei ameweka wazi kuwa, mkataba huo una malengo makuu mawili ikiwa ni kufanikisha suala la kuboresha hali ya lishe na kupunguza athari za utapiamlo na kuhakikisha jamii inashiriki ipasavyo kupanga, kutekeleza na kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa mpango wa halmashauri wa afua za lishe.

Amesema kuwa kwa kuzingatia malengo hayo Maafisa Watendaji ambao ni wasimamizi wapaswa kufanya kazi hiyo kwa weledi kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa, kulingana na vigezo na viashiria 9 vilivyoanishwa kwenye mikataba .

"Kila mtu anafahamu umuhimu wa afya bora katika maisha ya binadamu na ujenzi wa Taifa, Serikali imewapa jukumu hili muhimu, nendeni mkalitekeleze  kwa umakini mkubwa kulingana na makubaliano, kama kuna changamoto tushirikishane kwa wakati ili kwa pamoja tufikie malengo yaliyokusudiwa na serikali". Amesisitiza Kaimu Mkurugenzi huyo.
 
Naye Mratibu wa Lishe, halmashauri ya Arusha, Doto Milembe, amefafanua kuwa, Mkataba wa lishe unawataka Maafisa Watendaji wa Kata kuhakikisha wanashirikiana na  Maafisa Watendaji vijiji, kufanya kazi hiyo pamoja na kufanya tathmini na kutoa ripoti ya utekelezaji kwa kila mwezi.

"Lishe duni inanikusababisha umasikini katika Taifa kwani hakutakuwa na Jamii inayoweza kujituma kwa kufanya kazi kutoakana na watu wengi  kuathiriwa na utapiamlo, viongozi wenzangu tupambane kutokomeza utapiamlo katika maeneo yetu,,ili kuwa na watu wenye afya bora"Amesisitiza Mratibu huyo wa Lishe.

Nao Maafisa Watendaji wa kata, wameahidi kwenda kufanyia kazi maelekezo yote kama yalivyo malengo yake kwa kuzingatia vigezo na viashiria vilivyoainishwa kwenye mkata, ikiwa ni pamoja na kuifanya agenda ya kudumu kwenye vikao vyote vya kisheria.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Bwawani Simon Kaaya amebainisha kuwa, wao kama watendaji wanalo jukumu kubwa la kuutekeleza mpango huo kwa vitendo kwa kuwa unawahusu wananchi moja kwa moja ambao wako chini ya mamlaka zao za vijiji na vitongoji.

"Mpango wa lishe ni muhimu kwa kuwa tunakwenda kuandaa wananchi wenye afya bora ambayo ni nguvu kazi ya taifa, tutatumia majukwaa yote kutoa elimu kwa makundi kwa kushirikiana na wahudumu wa afya ngazi ya jimii na kuhakikisha unakuwa na matokeo chanya" Amesisitiza Kaaya.

Ifahamike kuwa mkataba wa Lishe ni mkakati wa Kitaifa ambao ulisainiwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan  jijini Dodoma na baaye kusainiwa na wakurugenzi wa hamashauri kupitia ofisi ya Mkuu wa mkoa na hatimaye, kusainiwa na halmashauri ya Arusha.


Arusha DC 

KaziInaendleeo ✍✍



PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA KUSAINI MKATABA WA LISHE




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.