Na Elinipa Lupembe
Jumla ya watoto elfu 80, wenye umri wa miaka 5 mpaka miaka 14, halmashauri ya Arusha wanategemewaa kupatiwa dawa za kinga tiba dhidi ya minyoo tumbo, dawa zitakazotolewa kwenye shule zote za msingi za halmashauri hiyo.
Dawa hizo zinatolewa kwa watoto wa umri huo, ikiwa ni mpango wa kitaifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, kwa watoto wote wa umri huo, walio kwenye mfumo wa shule na wale wa nje ya mfumo wa shule.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Arusha, Dkt. Petro Mboya, amethibitisha kukamilika kwa maandalizi ya utoaji wa dawa hizo za minyoo, ikiwemo kutoa elimu kwa walimu wa afya shuleni, na wahudumu wa afya ngazi ya jamii, wanaokwenda kugawa dawa hizo kwa watoto.
Aidha Dkt. Mboya, amefafanua kuwa makusudi ya mpango ni kuendeleza mpango jumuishi wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ukiwa na dira ya kuwa na jamii yenye afya bora na ustawi na usiyodhoofisha na madhara ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.
Naye Mratibu wa Magonjwa yasiyo ya kuambukizwa halmashauri ya Arusha, Ramadhani Kulewa, amesema kuwa halmashauri inategemea kutoa kinga tiba hiyo kupitia vituo 211, ikiwa shule za msingi 155, vituo vya afya 56, huku wahudumu 433 wakigawa dawa hiyo ambapo walimu ni 310 na wahudumu wa afya 112.
Kulewa aethibitisha kuwa ili kufikia lengo, licha ya kuwa na vituo hivyo maalum halmashauri pia itatumia mfumo wa ugawaji dawa katika jamii kwa kupita nyumba kwa nyumba, ugawaji wa dawa kwa makundi maalum, pamoja na kwenye mikusanyiko ya watu kama nyumba za ibada, sokoni, vituo vya mabasi na meeneo yote ya biashara.
Awali halmashauri ya Arusha inategemea kuwapatia kinga tiba ya minyoo kwa watoto 80,000, watoto 76,000 kati yao ni wale waliosajiliwa shuleni na watoto 4,000 ni ambao hawajasajiliwa kwenye mfumo rasmi wa elimu.
ARUSHA DC
KaziInaendelea ✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.