• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATOTO WALALAMIKIA WAZAZI KUSHINDWA KUWAANGALIA; CHANZO CHA ULAWITI KWA WATOTO WA KIUME

Posted on: October 30th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Watoto wa kiume shule za msingi, wamebainisha kuwa chanzo kikubwa cha ulawiti kwa watoto wa kiume ni wazazi kushindwa kuwasimamia watoto wao katika malezi kwa kujikita zaidi kwenye kwenye mambo yao na kuwaacha watoto wakijilea wenyewe.

Watoto hao wametoa maoni hayo wakati wa midahalo ya kutoa elimu ya Ulawiti, iliyofanyika baina ya Kamati ya Kupinga Ukatili wa Ulawiti kwa wavulana 'Father on Duty' na klabu za Maabara za  wavulana shuleni (Boy's Vac Lab), mdahalo uliofanyika kwenye shule 4 za msingi halmashauri ya Arusha.

Watoto wameelekeza malalamiko yao kwa wazazi  kwa kueleza kuwa baadhi ya wazazi wamepoteza maadili kwa kufanya mambo mabaya mbele ya watoto na  wengine kujikita zaidi kwenye kutafuta pesa za kuendesha maisha na kuwaacha watoto wakijilea wenyewe majumbani.

Hansa Masawe mwanafunzi (VI) shule ya msingi Ilboru, amebainisha kuwa baadhi ya wazazi na watu wazima hufanya vitendo vya ngono huku watoto wakiona jambo ambalo linawafanya watoto nao kuiga na kuanza kufanyiana wenyewe kwa wenyewe.

Lomnyaki Mollel mwanafunzi (5) shule ya msingi Olturoto amebainisha kuwa kwa sasa wazazi wanatumia muda mwingi kutafuta pesa za kuendeshea maisha na kuwacha watoto chini ya uangalizi wa ndugu, jamaa na marafiki, watu hao huanza kuwalawiti watoto na watoto huzoea na kuanza kufanyiana wenyewe kwa wenyewe.

Nasiri Shaban mwanafunzi wa shule ya msingi Naurei,  ameeleza kuwa, tabia ya wazazi kuacha watoto wanalala na wageni wajapo nyumbani nayo ni chanzo cha ulawiti kwa watoto wa kiume, na kuwataka wazazi kuwacha tabia ya kuwalaza wageni kwenye vyumba vya watoto.

Hata hivyo wanavulana hao wamelalamikia, kitendo cha jamii kuwatetea watoto wa kike na kuwaacha watoto wa kiume kando, kimesababisha wakatili kugeukia kwa watoto wa kiume, madhara yake yameanza kuonekana, hivyo jamii inapaswa kuelekeza nguvu pia kupambana na ukatili dhidi ya watoto wa kiume hususani kwenye vitendo vya ulawiti.

Mratibu wa Kuthibiti Maambuki ya UKIMWI Halmashauri ya Arusha, Dkt. Japhet Champanda, ameeleza madhara ya watoto kulawitiwa kiafya ni pamoja na kushindwa kuzuia haja kubwa, kupata mamabukizi ya magonjwa ya zinaa ambayo ya kiiingia sehemu ya haja kubwa ni vigumu sana kutibika.

"Athari za ulawiti, humuondrlea mwanaume urijali na kuathirika kisaokolojia kwa kushindwa kujiamini na kushindwa kutekeleza majukumu yake kama mwanaume" .Amesisitiza Dkt. Champanda.

Hata hivyo wajumbe wa kamati ya Father on Duty amewataka wamewataka watoto kukataa kuingiliwa na wanaume wenzanzao na kutoa taarifa pale wanapohisi mtu mwenye nia ovu ya kuwafanyia vitendo hivyo, pamoja kutoa taarifa za siri kwa walimu kama kuna watoto wanafanyiana vitendo hivyo.

Halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na shirika la CWCD, linatekeleza mradi wa kupinga ukatili wa kingono na ulawiti kwa watoto wa kiume, kupitia  maabara za wavulana 'Boy's Vac Lab' katika shule za msingi za Naurei,  Moivo, Ilboru, Olturoto, Kiranyi na Ngaramtono kwa ufathili wa Foundation for Civil Society.


ARUSHA DC

KaziIendelee✍✍













Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.