KARIBU watu 172,000 walijitokeza kuomba nafasi za ajira 21, 200 zilizotangazwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kada za Ualimu na Afya, serikali imesema.
Waziri wa Tamisemi, Angellah Kairuki amesema leo jijini Dodoma kuwa jumla ya maombi 171,916 yakiwemo ya Wanawake 76,190 na Wanaume 95,726 yalipokelewa kwenye mfumo, ambapo maombi ya Kada za Afya yalikuwa ni 48,705 na Kada ya Ualimu ni 123,211.
Serikali ilitoa kibali cha ajira za kada ya afya 8,070 na wengine 13,130 kwa ajili ya kada ya ualimu.
Hata hivyo iorodha ya majina ya waombaji waliopangiwa vituo imeonesha watu 5,319 kati ya 48,705 ndio waliopata ajira kati ya nafasi 8,070 zilizotangazwa.
Kairuki amesema Waajiriwa wapya ambao hawataripoti katika vituo walivyopangiwa ndani ya siku 14 kuanzia tarehe ya tangazo hili, watakuwa wamepoteza nafasi zao na nafasi hizo zitajazwa na waombaji wengine wenye sifa waliopo kwenye Kanzidata (Database) ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI.
Una maoni, tuandikie
Bofya hapa kutazama Majina kwa Pdf
#HabarileoUPDATES
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.