• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI SEKTA YA AFYA WAKUMBUSHWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KATIKA KAZI

Posted on: August 4th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Watumishi sekta ya Afya wamekumbushwa kutekeleza majuku yao ya kazi, huku wakizingatia kanuni na taratibu za utumishi wa Umma, ili kufikia lengo la serikali la kiwahudumia wananchi.


Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Idara ya Utumishi na Rasilimali watu, halmashauri ya Arusha, Elizabeth Ngobei alipokutana na watumishi wa hospitali ya Selian Ngaramtoni, kwenye kikao kazi cha kujadili masuala mbalimbali ya kiutumishi hususani katika masuala ya haki na wajibu wa mtumishi wa Umma katika eneo lake la kazi.


Mkuu huyo wa Idara ya Utumishi, amewataka watumishi hao, kutambua kuwa, katika utumishi wao wa Umma, wanapaswa kutambua wanayodhamana kubwa ambayo Serikali imewaamini hivyo wana wajibu wa kutekeleza majukumu yao ya kitabibu ili kufikia lengo la serikali la kuwahudumia wananchi katika sekta hiyo ya Afya.


Elizabeth amewasisitiza kuwa, kila mtumishi anapaswa kutambua haki na wajibu wake unaozingatia maadili ya taaluma yake kazini na si vinginevyo na kuongeza kuwa serikali inapotoa haki ya kuajiri na kulipa mshahara mtumishi, mtumishi pia anaowajibu wa kutekeleza majukumu yake  kutokana na haki hiyo anayopewa na serikali.


"Licha ya kazi ngumu mnayoifanya watumishi wa sekta hii ya afya,  Serikali inatambua na kuthamini kazi yenu, hivyo ni vema kila mtumishi kufanya kazi kuendana a kasi ya maendeleo na kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazoea" Amesisitiza Afisa Utumishi huyo


Hata hivyo Elizabeth amewashauri watumishi hao, kujiendeleza kielimu kupitia taaluma walizoajiriwa nazo, ili kuongeza ufanisi katika kazi unaoendana na mabadiliko ya Sayansi na teknolojia pamoja na kupanda madaraja na ngazi za mshahara.


Nao watumishi wa hospitali ya Serilan wameipongeza uongozi wa halmashauri hiyo, kupitia Idara ya Utumishi kwa kukutana na watumishi hao na kufanya kikao ambacho kimewapa uelewa na ufahamu mkubwa kwenye masuala ya utumishi wa Umma, pamoja na kuwajengea uelewa wa pamoja juu ya haki na wajibu wa watumishi katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.


Asaria Giliad Mhudumu wa Afya hospital ya Selian, ameweka wazi kuwa, kikao hicho kimekuwa na matokeo chanya kwao, kwa kuwa wamepata fursa ya kuwa na uelewa wa pamoja kati ya mwajiri na mtumishi, sambamba wajibu wa mtumishi katika utekelezaji wa majukumu yake ya kazi.


"Tumepata fursa ya kukumbushana mambo mbalimbali ya kiutumishi, ikiwemo masuala ya miundo ya utumishi, upandaji wa madaraja, michango ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na mafao ya kustaafu, mambo ambayo watumishi wengi yalikuwa yanatuchanganya" Amebainisha Elias Molle dreva wa Hospitali hiyo


Naye Mkurugenzi wa Hospitali ya Seliani Dkt. Amon Marti, licha ya kupongeza uwepo wa kikao kazi hicho, amewataka watumishi kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa Umma ikiongozwa na nidhamu inayoongozwa na uzalendo ili kufikia malengo ya serikali ya kuwahudumia wananchi.

Awali Hospitali ya Selian ni miongoni mwa hospitali  za halmashauri ya Arusha, inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi ya Kaskazini, ikiwa na jumla ya watumishi 111 wanaolipwa mishahara na serikali kupitia ruzuku, kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wanachi.


SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022

JIANDAE KUHESABIWA✍✍✍

Mkui wa Idara ya Utumishi, halmashauri ya Arusha Elizabeth Ngobei, akizungumza na watumishi wa hospitali ya Selian Ngaramtoni wakati wa kikao kazi, kilichofanyika kwenye ukumbi wa kanisa la hospitali hiyo

Watumishi wa hospitali ya Selian Ngaramtoni wakifuatilia mada zilizotolewa wakatii wa kikao kazi, kilichofanyika kwenye ukumbi wa kanisa la hospitali hiyo


Mhudumu wa afya hospitali ya Selian Ngaramtoni, Isaria Giliard akiuliza swali juu ya haki za mtumishi katika  mafao ya kustaafu, wakati wa kikao kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa kanisa ndani ya hospitali hiyo. 


Baadhi ya Watumishi wa hospitali ya Selian Ngaramtoni wakifuatilia mada zilizotolewa wakatii wa kikao kazi, kilichofanyika kwenye ukumbi wa kanisa la hospitali hiyo

Baadhi ya Watumishi wa hospitali ya Selian Ngaramtoni wakifuatilia mada zilizotolewa wakatii wa kikao kazi, kilichofanyika kwenye ukumbi wa kanisa la hospitali hiyo





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.