• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI WATAKIWA KUWEKA UTARATIBU WA KUPATA CHAKULA KWA KUZINGATIA VIRUTUBISHO VYA MAKUNDI MATANO YA CHAKULA WAWAPO MAKAZINI

Posted on: July 4th, 2021

Na .Elinipa Lupembe.

Watumishi wa Umma wametakiwa kupanga namna ya kupata lishe bora wawapo kazini, kwa kuhakikisha wanapata chakula chenye virutubisho vinavyotokana na makundi matano ya vyakula kutokana na muda wao wa kula kuwa finyu kutokana na mazingira halisi ya muda wa kazi.

Hayo yamesemwa na Mganga mkuu wa Jiji la Arusha, Dkt. Kheri Kagija wakati akifunga mafunzo ya  Afya katika sehemu za kazi, yaliyowakutanisha wawakilishi wa kamati za Lishe, Maafisa Lishe na Maafisa Ugani wa halmashauri za  mkoa wa Arusha, kikao kilichofanyika kwenye hoteli ya Safari ya Jijini Arusha.

Dkt. Kagija amefafanua kuwa, maendeleo ya taifa lolote,  yanawategemea wafanyakazi, ambao wantumia nguvu nyingi kufaya kazi, nguvu ambazo zinategemea afya bora, hivyo ni vema wafanyakazi wakapata chakula bora, chenye virutubisho vyote vinavyotkana na makundi matano ya chakula kila mlo wanaoupata wawapo kazini.

Aidha Dkt. Kagija amewataka Maafisa Lishe wa halmashauri zote kutoa elimu kwa wafanyakazi, itakayowawezesha kuwa na ratiba nzuri ya chakula katika maeneo yao ya kazi, chakula chenye virutubisho vyote lengo likiwa ni kunusuru afya za watumishi wa Umma.

Ameweka wazi  kuwa ulaji wa wafanyakazi wawapo kazini, umekuwa ni chanzo cha kudhoofisha sana afya zao na kujikuta wengi wao, wakishambuliwa na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwemo, kisukari, shinikizo la damu, vitambi, baridi yabisi pamoja na utapiamlo uliozidi bila kufahamu maradhi hayo yanatokana na ulaji mbovu wanoufanya wawapo kazini.

"Ni kawaida kukuta mfanyakazi asubuhi anapata supu chapati na soda,  chai chapati ama maandazi, kwa wiki nzima, huku mchana akilazimika kula ugali ama wali nyama, chipsi mayai na mishikaki ama nyama choma na ndizi, vyakula ambavyo kwa asilima kubwa vinaangukia kwenye kundi moja ama mawili tuu ya vyakula" amefafanua Dkt. Kagija.

Naye Meneja Mkuu wa Mradi wa shirika la  Global Alliance for Improved Nutrition 'GAIN' Dkt. Winfrida Mayilla, ameongeza kuwa ni vema kutoa  elimu ya lishe kwa wafanyakazi kwa kuwa wanatumia muda mwingi kazini huku ratiba zao za kula zikiathiriwa na muda na mazingira, kupitia elimu ya lishe, wafanyakazi wanaweza kujenga tabia ya kupata chakula chenye virutubisho, jambo ambalo litaimarisha afya za wafanyakazi.

"Wafanyakazi wanatakiwa kuzingatia ulaji mzuri wa chakula, chakula ambacho kitakuwa ni mlo uliobeba virutubisho vinavyotoka na makundi yenye mchanganyiko wa nafaka, matunda, wanyama na mikunde, mbagamboga na mafuta." Amesema Dkt. Winifrida.

Hata hivyo washiriki wa mafunzo hayo, wakiwemo Maafisa Lishe, wamethibitisha ulaji mbovu wa watumishi wawapo kazini, kutokana na kutumiamjuda mrefu kazini na kukosa muda wa kuandaa chakula chenye virutubisho vinavyotokana na makundi matano ya chakula, na kujikuta wakila vyakula vya aina moja kwa muda mrefu, jambo linalowasababishia kuwa na afya duni

Afisa Lishe halmashauri ya Arusha, Doto Milembe, amethibitisha kuwepo na tabia hasi za ulaji kwa wafanyakazi kutokana na uelewa mdogo wa masuala ya ulaji, na kuongeza kuwa wanajukumu la kutoa elimu kwa watumishi pamoja na kuwapima uzito mara kwa mara,  ili waweze kujua afya zao na kuanza kula chakula chenye virutubisho vyote wawapo kazini.

Mafunzo hayo ya siku moja yamekutanisha maafisa Lishe,maafisa Ugani, maafisa Afya pamoja na na wajumbe wa kamati za Lishe kutoka halamshauri saba za mkoa wa Arusha.

Arusha 

Kazi inaendelea✍✍






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.