• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAWAKILISHI WA VYAMA VYA SIASA ARUMERU MAGHARIBI WAKABIDHIWA RATIBA NA VITINI VYENYE MAELEKEZO YA UCHAGUZI MKUU

Posted on: August 11th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

       Wawakilishi wa Vyama vya siasa vitakavyoshiriki Uchaguzi Mkuu, Jimbo la Arumeru Magharibi wamekutana na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Arumeru Magharibi na kufanya kikao, kwa ajili ya kupeana taratibu za mchakato mzima wa Uchaguzi Mkuu, unaotarajia kufanyika tarehe 28 Oktoba, 2020.

       Katika kikao hicho, kilichofanyika kwenywe Ofisi ya Uchaguzi halmashauri ya Arusha, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Arumeru Magharibi, Saad Mtambule, amewataka wawakilishi hao wa Vyama vya Siasa kuzingatia Kanuni, sheria na taratibu zinazoelekezwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ambao ndio msingi wa uchaguzi ulio huru na haki.

      Amefafanua kuwa, miongozo ambayo imeandikwa kwenye vitini vilivyoandaliwa na Tume na kugawiwa kwa wawakilili wa vyama vyote vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, imelenga  kuwa na uchaguzi huru, haki, uwazi na kuaminika, wenye kuzingatia ushiriki wa makundi wa makinsi yote ya jamii na watanzania wote

        Mtambule amewasisitiza Wawakilishi hao wa vyama vya siasa, kushirikiana na Tume ya Uchaguzi, kuwaelimisha wananchi hasa wafuasi wa vyama vyao, kufahamu haki na wajibu wao katika uchaguzi mkuu, ili kuwa na uelewa wa pamoja, utakaowezesha uchaguzi kuwa wa amani, huru na wa haki.

     "Ili Uchaguzi Mkuu uwe wa amani, ni jukumu letu wasimamizi wa Uchaguzi na ninyi wawakilishi wa vyama na  wafuasi wa vyama vyenu kujenga nidhamu na kuheshimu taratibu zinavyoelekeza, waelimisheni wanachama wenu kutambua hilo kipindi chote cha Uchaguzi, ili Uchaguzi uwe wa amani kwa maslahi ya watanzania wote" amesisitiza Mtambule.

        Aidha amawataka wawakilishi hao wa vyama, licha ya kufuata kanuni na taratibu, amewakumbusha kuzingatia  ratiba waliyokabidhiwa, waweze kuendana na muda na matukio yaliyoelekezwa kwa wakati husika, lengo likiwa kuepuka malalamiko yasiyokuwa ya lazima katika kipindi chote cha Uchaguzi.

      Hata hivyo wajumbe hao wamekubaliana kufanya mchakato wa uchaguzi kwa amani na utulivu na kuweka maslahi ya watanzania mbele, huku wakimuomba Msimamizi wa Uchaguzi, kusimamia uchaguzi uwe huru na haki, huku wakisisitiza kuwa maisha ya watanzania ni zaidi ya uchaguzi kwa kuwa  kuna maisha baada ya uchaguzi.

    Awali Wawakilishi hao wa Vyama vya Siasa, wamekabidhiwa vitini vya miongozo mbalimbali ya Uchaguzi Mkuu  pamoja na Ratiba ya mchakato mzima wa Uchaguzi kama ilivyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.










Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.