• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI  WATAKIWA KUPAMBANA NA UKATILI WAKINGONO KWA WATOTO WA KIUME

Posted on: December 9th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wazazi na walezi wametakiwa kuamka na kuanza harakati madhubuti za kupambana na ukatili wa kingono dhidi ya watoto wa kiume, kama inavyofanyika  kwa watoto wa kike kwa kipindi kirefu sasa.

Rai hiyo imetolewa na Afisa Maendeleo ya Jamii, Dawati la Jinsia, Rovil Nguyaine, wakati wa kikao kazi kilichojumuisha wajumbe wa Kamati ya MTAKUWWA ngazi ya kata kutoka kata 6 za halmashauri ya Arusha,  kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Nguyaine  amebainisha ongezeko la kasi la matukio ya ulawiti kwa watoto wa kiume, watoto ambao wazazi na jamii hawakushughulika nao kwa dhana ya kuwa wanao uwezo wa kujitetea kiume, jambo ambalo madhara yake yameanza kuonekana sasa.

Ameongeza kuwa ni jukumu la wazazi na jamii, kuhakikisha wanawalinda watoto wote dhidi ya ukatili wa kijinsia na sio watoto wa kike peke yao, kwa kuwa watoto wote ni sawa na wanahitaji kulindwa kuanzia nyumbani, njiani mpaka shuleni.

 "Wazazi/ Walezi jengeni desturi ya kushirikiana na walimu katika kupambana na ukatili wa kijinsia, hakikisheni mnakuwa karibu na watoto wenu, kwa kuwa hali ya ukatili ni mbaya sana hasa kwa wtoto wa kiume". Amesema Ngutaine

Hata hivyo wajumbe hao wa kamati ya MTAKUWWA licha ya kushukuru kikao kazi hicho, wamethibitisha uwepo wa matukio ya ukatili kwa watoto wa kiume na kuahidi kuendelea kuhamisisha jamii kujikita kupambana na ukatili kwa watoto wote wa kike na wa kiume.

Wameongeza kuwa, kupitia mafunzo wanayopewa na serikali na mashirika juu ya ulinzi na usalama wa watoto, umewezesha jamii kuanza kuwa na uelewa wa pamoja juu ya usimamizi wa usalama na haki za watoto, sambamba na namna ya kushughulikia matukio ya ukatili pindi yanapotokea.

Naye mjumbe wa Kamati ya MTAKUWWA kata ya Moivo Elizabeth, amelilalamikia jeshi la Polisi kuwa na vikwazo wakati wa ufuatiliaji wa kesi za ukatili na kuweka wazi kuwa, kutokana na ukiritimba uliopo,  unasababisha wengi kurudi nyuma kwa kukataa tamaa kutokana na usumbufu.

Hata hivyo Mratibu wa Dawati la Jinsi, na Mpelezi wa kesi za Ukatili, Kituo cha Polisi Ngaramtoni,  Koplo Jane Mandi  amewataka wazazi na wajumbe wa MTAKUWWA kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa matukio yoyote ya ukatili pamoja nakufuata taratibu ambazo zitawezesha kesi kufika mwisho na hatimaye watoto kupata haki zao.

"Jeshi la Polisi liko tayari kushirikiana na kamati za MTAKUWWA kwa matukio yote ya ukatili na kuhakikisha watuhumiwa wanatiwa hatiani na kujitoa kutoa ushahidi kwenye kesi ili watoto  waweze kupata haki zao, kwa sasa Jeshi la Polisi linasimamia kwa uwazi haki za watoto.

Koplo Jane amezungumzia  mila na desturi za jamii bado ni kikwazo cha kesi nyingi za ukatili kutoka na ukweli kwamba matukio hayo yanatokea ndani ya familia na kusababisha wahanga kuogopa kutengwa na familia zao.

Awali Mratibu wa Mradi wa Kupinga Ukatili wa Kingono dhidi ya Watoto wa kiume, Shirika la CWCD, Mariam Rashid amesema kuwa lengo la kikao kazi hicho ni kukumbushana majukumu kwa wajumbe wa kamati ya MTAKUWWA na kuwashirikisha kushiriki mradi wa ukatili wa kingono kwa wavulana unaonedelea kwenye kata zao.

Halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na shirika la Center for Women and Children Develepment ( CWCD), wanatekeleza mradi wa kupinga ukatili wa kingono kwa watoto wa kiume kwenye kata 6, kwa ufadhili wa Foundation for Civil Society.


ARUSHADC

KaziIendelee✍



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.