• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZEE ARUSHA DC WAADHIMISHA SIKU YA WAZEE, HUKU WAZEE 11,076 WAKIWA NA VITAMBULISHO VYA MATIBABU YA WAZEE

Posted on: October 5th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Wazee halmashauri ya Arusha, wameungana na wazee wote, kuadhimisha siku ya Wazee Duniani, huku jumla ya wazee 11, 076 wakiwa tayari wana vitambulisho vya matibu ya Wazee, maadhimisho yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri ya Arusha.

Taarifa hiyo imethibitishwa na mgeni rasmi na mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mheshimiwa Mhandisi Richard Ruyango, kuwa wazee wa halmashauri hiyo, wameadhimisha siku hiyo maalum kwao, wakati halmashauri ikiwa imefanikiwa kuwawezesha jumla ya wazee 11, 076 kati ya wazee 12,892 waliotambuliwa.

Mkuu  wa wilaya Ruyango amefafanua kuwa, serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na mheshimiwa Rais mama Samia Suluhu Hassan, inatambua thamani kubwa ya wazee waliotumikia taifa la Tanzania katika kipindi cha maisha yao, zaidi inatambua mchango wa wazee katika maendeleo ya Taifa hili, hivyo inaendelea kuboresha miundombinu ya huduma kwa wazee, na kuhakikisha wazee wanaendelea kupata huduma bora, lengo likiwa ni kuwafanya kuendelea kuishi kwa amani na utulivu, huku wakifurahia matunda ya nchi yao.

Aidha mkuu huyo wa wilaya amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wazee, kwa kuwepo na dirisha maalumu la kutibiwa wazee kwenye kila kituo cha kutolea huduma za afya, ili kuwaharakishia upatikanaji wa huduma za matibabu, mara wazee wanapofika kwenye kituo vya afya.

"Mkurugenzi na Mganga mkuu, hakikisheni kila kituo cha afya kuna dirisha la Wazee, lakini ikiwezekana apangwe muhudumu wa afya, maalumu wa kuwahudumia wazee, pindi wanapofika kupata matibabu, ili wasikae muda mrefu wakati wa kupata huduma za matibabu". Amesisitiza Mheshimiwa Ruyango.

Hata hivyo wazee hao wamewasilisha changamoto zinazowakabi ikiwa ni pamoja na kulea wajukuu ambao ni yatima na wengine kutelekezwa na wazazi wao, pamoja na baadhi ya wazee wasiokuwa na vitambulisho vya matibabu ya wazee kukosa matibabu pindi wanapougua, pamoja na Viongozi wa Baraza la  wazee kutokuwa na ofisi maalum ya kuwahudumia wazee.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee halmashauri ya Arusha, Mzee Elias Ngungati amemshukuru mkuu wa wilaya ya Arumeru kupitia ofisi ya mkurugenzi na watalamu wa halmashauri ya Arusha kwa kuwajali wazee, pamoja na changamoto zinazowakabili wazee, lakini halmashauri imeendelea kuboresha maslahi mbalimbali ya wazee kupitia  Baraza la wazee la halmashauri mpaka kuwafikia kwenye ngazi ya kata.

"Licha ya kuwa bado kuna changamoto zinazowakabili lakini serikali inaendela kufanya maboresho tofauti na hapo awali, na kusisitiza kupewa ofisi ya viongozi wa Baraza la Wazee ili kurahisiha upatikani wa viongozi pindi wazee wanapotaka kukutana na kujadili mambo yao" amesisitiza Mwenyekiti Ngungati.

Awali mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amekiri kutambua na kupokea changamoto zilizowasilishwa na wazee hao, na kuahidi kuzifanyia kazi na kutatua baadhi ya kero hizo kwa awamu, kulingana na upatikanaji wa fedha na kusisitiza kusimamia upatikanaji wa huduma za haraka za afya kwa wazee,  kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya pamoja na kutafuta namna ya kuwapatia viongozi wa Baraza la Wazee ili kurahisisha ukutanaji wao.

"Ninatambua changamoto za wazee ni nyingi, lakini halmashauri inaendelea kuzitatua na kuzipunguza kwa awamu, sambamba na kupatikana kwa ofisi za uongozi wa Baraza la Wazee" amesistiza mkurugenzi Msumi.

Katika maadhimisho hayo, idara ya Afya ilifanikiwa kutoa elimu ya ugonjwa hatari wa Covid 19 (UVIKO 19) kwa kuwataka wazee kupata chanjo ya UVIKO19 pamoja na kuendela kujihadhari na ugonjwa huo hatari.

Maadhimisho hayo ya  siku ya Wazee Duniani hufanyika tarehe 01, Oktoba kila mwaka, huku halmashuri ya Arusha, ikiadhimisha kwa kuhusisha Baraza la Wazee pamoja na Wazee wawakilishi kutoka kata zote 27 za halmashauri ya Arusha,  maadhimisho hayo yamefanyika kwa ushirikiano wa halmashuri na wadau wa maendeleo wa shirika la DORCAS na CWCD, yakiwa na kauli mbiu  Mbiu ya siku ya Wazee 2021:  "MATUMIZI SAHIHI YA KIDIGITALI KWA USTAWI WA RIKA ZOTE"


MATUKIO KATIKA PICHA.


Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mheshimiwa mhandisi Richard Ruyango akizungumza na wazee, wa halmashauri ya Arusha wakati wa maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani, maadhimisho yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri hiyo.



Mwenyekiti wa Baraza la Wazee, halmashauri ya Arusha, akisoma risala ya Wazee, mbele ya mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mheshimiwa mhandisi Richard Ruyango wakati wa maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani, maadhimisho yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri hiyo.


Baadhi ya Wazee halmashauri ya Arusha, wakifuatilia mijadala mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani, maadhimisho yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri hiyo.


Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani, maadhimisho yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri hiyo.


Baadhi ya Wazee halmashauri ya Arusha, wakifuatilia mijadala mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani, maadhimisho yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri hiyo.


Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mheshimiwa mhandisi Richard Ruyango akikabidhiwa Rungu na Wazee wa halmashauri ya Arusha, ikiwa ni ishara ya kumtawaza kuwa mlezi wa Wazee, wakati wa maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani, maadhimisho yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.