• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZEE ARUSHA DC WAHIMIZWA KUSHIRIKI VIKAO VYA MABARAZA YA WAZEE

Posted on: October 2nd, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wazee halmashauri ya Arusha, wamehimizwa kushiriki vikao vya mabaraza ya wazee, kuanzia ngazi ya kata, lengo likiwa ni kutekeleza sera ya Taifa ya wazee ya mwaka 2003 na sera ya Afya ya mwaka 2007, zikiwa na lengo la kuhakikisha Ustawi wa wazee nchini, vikao ambavyo vitawezesha  kuweka mipango thabiti ya kukabiliana na changamoto zao  pamoja na kuimarisha uhusiano baina yao.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi na Afisa Utumishi Mkuu, halmashauri hiyo, Elizabeth Ngobei, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani kiwilaya, sherehe zilizofanyika kwenye viwanja vya makao makuu ya halmashauri hiyo na kuwataka kufahamu kuwa vikao vya mabaraza ya wazee ni vikao halali kisheria.

Kaimu Mkurugenzi huyo amesema kuwa serikali imeandaa utaratibu wa kuunda mabaraza ya wazee kuanzia ngazi ya kata, ikiwa ni njia ya kukutana na kubaini changamoto zinazowakabili na kisha kuziwasilisha ngazi ya wilaya na hatimaye Taifa ili serikali iweze kuweka mipango ya kuzitatua changamoto hizo.

"Vikao ndio utaratibu halali na sahihi wa kuwasilisha mambo yenu kwa Serikali, Serikali  hufanyia kazi maamuzi yatakayotokana na mihitasari ya vikao hivyo halali, vinginevyo mtaishia kulalamika na itakuwa ni vigumu kufahamu na kuzitatua changamoto zenu, hakikisheni mnafanya vikao hivyo kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa". Amesistiza  Elizabeth

Aidha, wazee walioshiriki kwenye Maadhimisho hayo, wamekiri kutambua changamoto za kutokufanya vikao vya mabaraza na kuahidi, kuanza kutekeza wajibu huo, kwa kutambua kuwa ni fursa kubwa waliyopewa na Serikali yao.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wazee, halmashauri ya Arusha Mzee Aloyce Mollel, amekiri kuwepo kwa changamoto ya ufanyikaji wa vikao vya mabaraza ngazi ya kata, jambo ambalo linakwamisha utatuzi wa changamoto za wazee na kuahidi kufuatilia na kuhakikisha vikao hivyo vinafanyika kwa mujibu wa sheria.

"Wapo baadhi ya wazee wanaishi kwenye mazingira magumu, kutokana na umasikini uliokithiri wanakosa lishe bora na kuishi kwenye makazi duni, tukikutana kwenye vikao na kuweka mawazo yetu pamoja, tutapata namna bora ya kuwasaidia kutatua changamoto zetu na sio kulalamika". Amesema mzee Aloyce

"Wazee wenzangu, serikali inatujali, imetupa fursa ya kuwa na Mabaraza ya Wazee, tukutane tujadili na tupange mambo yetu, tusijifungie ndani, kukaa ndani tunajiongezea magonjwa, tutoke na kushughulisha miili na akili zetu, ni afya kwa kufanya hivyo itatuongezea siku za kuishi" Amesisitiza Ndekusura Mwenera kata ya Moivo

Hata hivyo wazee hao wamekiri kuwa, licha ya changamoto nyingi zinazowakabili, wameadhimisha siku hiyo, huku wakiwa na matumaini na serikali ya awamu ya sita kwa chukua hatua katika kuboresha huduma za afya sambamba na kuwatambua wazee na kuwapa vitambulisho vya wazee.

"Tunaishukuru serikali kwa kuweka utaratibu wa kuongeza bajeti ya dawa, uwepo wa dirisha maalum la matibabu kwa wazee, tunaiomba serikali kutusaidia dawa za magonjwa yasiyoambukiza yanayowakabili wazee". Amesema  Rose Mollel

Halmashauri ya Arusha imeazimisha siku ya wazee duniani yenye kauli mbiu ya 2022 yenye Kauli Mbiu ya " Ustahimilivu na Mchango wa Wazee ni Muhimu kwa Maendeleo", ikiwa imefanikiwa kuwatambua wazee 12, 892 kwa ajili ya kupatiwa huduma, huku  wazee 11,076 wakipatiwa vitambulisho vya wazee sawa na asilimia 100.

Maadhimisho hayo yaliambatana na burudani za muziki wa zamani, mashindano ya kucheza muziki na wazee kuelezea kumbukumbu muhimu katika masha yao, sambamba na wazee kupata huduma ya kupima afya kwa magonjwa yasiyoambukiza.



'Uzee na Kuzeeka, Hakuna wa Kukwepa'


PICHA ZA MATUKI SIKU YA MAADHIMISHO


Kaimu Mkurugenzi na Afisa Utumishi Mkuu, halmashauri ya Arusha, Elizabeth Ngobei, akihutubia wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani,sherehe zilizofanyika kwenye viwanja vya makao makuu ya halmashauri hiyo.


Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wazee, halmashauri ya Arusha Mzee Aloyce Mollel, akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani,sherehe zilizofanyika kwenye viwanja vya makao makuu ya halmashauri hiyo.


Baadhi ya Wazee walioshiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniami halmashauri ya Arusha











Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.